Habari za Punde

Makala ya Kuzaliwa kwa Mtume (SAW)

Na.Asia Hakim  MUM
Leo waislam wote duniani wanaadhimisha uzao wa Kiongozi wa Dini tukufu ya kiislam Mtume Muhammad (S.A.W) hakuna budi angalau tukajikumbusha historia ya mtume japokwa ufupi.
Kutoa historia katika makala hii haina maana kuwa waislamu hawaijui historia ya Mtume, au muandishi  anajua sana kuhusu hili. Bali ni vyema kukumbushana pindi nafasi inapotokezea.
Kiukweli unapo fuatilia historia ya Mtume (S.A.W) kuna mazingatio makubwa hususan katika maisha ya kila siku ya Muislam.
Katika makala hii itagusia kwa ufupi historia ya Mtume kutoka kuzaliwa hadi kufikia kupewa utume.

Kuzaliwa Kwake.
Mtume Muhammad (S.A W) alizaliwa mwezi 11 Mfungo sita alfajiri  ya kuamkia siku ya Jumatatu sawa na April 21 mwaka 571.ambayo ilinasibiana na tukio la ndovu na Mfalme Kisra(mwaka wa Tembo) ambapo ilikuwa ni mwaka wa 40 wa utawala wa Kisra. (Muhammad Suleiman, Najatul-Afham)
 Ibn Saad na  Musnad Ahmad akaeleza kuwa Kuzaliwa kwa mtume Muhammad (S.A.W) mbora wa viumbe vyote kulikua na Nuru  na baraka kubwa iliyo angaza duniani na ilikuwa ni ishara ya ukombozi wa jamii zote.

Ambapo mama yake Mtume (S.A.W) ameripotiwa akisema ‘wakati alipojifungua ulitoka mwaga mkubwa na kuelekea katika maeneo ya Syria na kuenea katika eneo lote’’
 Ambapo anaendelea kwa kusema Baada nuru hiyo kuenea Masanamu mbali mbali yaliporomoka na utawala wa Kisra ukaanguka pamoja na wachawi kupata fadhaa.

Ibn Hisham anaeleza kuwa baada ya babu yake Mtume (S.A.W) Bwana Abdul Mutallib kupata ishara njema ya kuzaliwa mtoto, alimchukua mjukuu wake  na kwenda nae hadi kwenye Al-kaaba kwa ajili ya kumuombea , na baadae kumpa jina la `Muhammad` na baada ya siku saba akamtahiri.

Furaha ya kuzaliwa kwa Mtume ilienea kwa familia nzima kwani pia Ami yake Abu Lahab  aliamua kumpatia mlezi Mtume Muhammad (S.A.W) ambae alikuwa mtumwa wake.
Mlezi huyo alikuwa Bibi Thuaiba ambae alikua ni mtu wa pili kumnyonyesha Mtume Muhammad (S.A.W) baada ya mama yake Mzazi Amina bint wahab.

Pia Mtume Muhammad (S.A.W)  alinyonyeshwa na Bi Halima ambae alimchukua kwa ajili ya kumlea jambo ambalo ilikuwa ni ada kwa waarabu kuwapeleka watoto wao kulelewa sehemu za mbali  ili waweze kuwa na Afya nzuri kutokana na hali mbaya ya hewa iliyokuwepo Makka.(sahihi Al-Bukhari).

Kwa mnasaba huo watoto waliweza kukuwa na afya nzuri na pia kujifunza lugha fasaha ya kiarabu  ambayo haikuchafuliwa na uingiliwaji wa lugha nyengine.

Ishara njema zilijitokeza mapema kwa Mtume Muhammad (S.A.W) tokea wakati wa kulelewa na Bi Halima  yaliyojitokeza kutokana na mabadiliko ya kiuchumi na maeneo mengine, mama huyu aliweza kunyonyesha watoto wengi kutokana na kujaa kwa maziwa  na hata ngamia wao aliyekuwa mgonjwa aliweza kutoa maziwa mengi.(zadul-maad uk 1/19)
Kutokana na bahati nzuri zilizojitokeza katika kumlea mtoto huyo Bi Halima alimuomba mzazi wake amuengezee  muda wa kukaa na mtoto huyo ili aendelee kupata kheri zake.

Abu Nuaim katika kitabu chake cha dalailun Annubuwah anasema, mtume Muhammad (S.A.W) Aliendelea kukaa na Bi Halima hadi alipofikia umri wa miaka minne.
imeoneshwa katika sahihi muslim kuwa alishuka Malaika Jibril na kumfanyia upasuaji wa kifua na kuutoa moyo wake na kuuosha katika maji ya Zam zam na baadae ukarejeshwa mahali pake.

Palikuwa na watoto walioweza kuliona tukio hilo na kwenda kumwambia mlezi wake, ambae alipatwa na wasiwasi na kuamua kumrejesha nyumbani kwao Makka.

Baada ya kurudishwa kwa mama yake mzazi Mtume Muhammad (S.A.W) aliishi na mama yake hadi umri wa miaka 6 ambapo mama yake alifriki dunia na kuzikwa katika kijiji cha Abwa kinacho pakana kati ya Makka na Madina baada ya kuugua.( Ibnu Hisham) 1/168
Baada ya hapo Mtume (S.A.W) alirudishwa kwa Babu yake  Abdul Mutallib Huko Makka  ambako aliishi nae kwa mapenzi makubwa  zaidi kuliko watoto wake  wote .

Ibni Hisham anaeleza kuwa kwa mapenzi aliyokuwa nayo babu kwa mjukuu wake  huyo ilifikia hadi kumruhusu Mtume (S.A.W) kusali mbele katika Al kaaba wakati yeye pia akisali. Wakati watoto wake walikuwa wakikaa nyuma ya baba yao kwa kumpa heshima.

Jambo hili hakuwahi kulifanya kwa mtoto wake yoyote, na aliye jaribu kumuondoa mtume (.S.A.W) mbele alikatazwa na kuelezwa kuwa ` mwacheni mjukuu wangu  huyu atakuja kushika nafasi kubwa`
Mzee  Abdul Mutallib alionekana kumuamini sana kijana wake kwani  alikuwa akimshirikisha katika mambo yake mengi  kutokana alikuwa akiridhishwa na vitendo vyake.

Wakati Mtume Muhammad (SAW) alipofikia umri wa miaka 12 alikwenda katika safari ya bishara na Ami yake Abu Talib  katika nchi ya Syria.

Walipofika katika kijiji cha (Busra) ambacho kilikuepo katika maeneo ya Syria lakini yakimilikiwa na Utawala wa Kiroma, katika kijiji hicho walikutana na Kasisi mmoja wa Kikristo aliyeitwa Bahira(George)
Baada ya kumuona Kasisi huyo alimtambua Mtume (S.A.W) na kumtaka Ami yake arudi nae huko Makka ili asije kudhuriwa na Watu wenye chuki dhidi yake. ( Ibni Hisham, Talqih fuhum Ahlil-afham).
Wakati Abu Talib alipotaka kujua ishara ya kijana yule kuwa ni Mtume wa Allah  Bahira alijibu ‘’wakati mlipotokea katika eneo hili miti yote na majabali yalianza kusujudu, jambo ambalo halijawahi kutokea isipokuwa kwa mitume wa Allah (SW).

Pia nimemtambua Kijana huyu kuwa atakuwa Mtume baada ya kuona muhuri wa Utume katika bega lake ambapo ishara hizi nimeziona katika kitabu chetu’’ (At.Tirmidhi no 3620).
Baada ya kupata maelezo hayo Abu Talib aliamua kumrudisha Mtume (S.A.W) Makka na yeye akaendelea na safari.
Wakati Mtume (S.A.W) akiendelea na maisha yake alijishughulisha na uchungaji wa wanyama waliotoka katika ukoo wa Banii saad ambapo alikuwa akichunga kwa malipo.
Alipofikia umri wa miaka 25 alikwenda Syria kwa ajili ya kufanya biashara za tajiri wake Bi Khadija.

Ibn Ishaaq anaeleza kuwa baada ya bibi Kadija kupata habari za kijana muaminifu katika maneno na vitendo, mnyenyekevu na mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri. Alivutiwa nae na kuamua kumuajiri awe mfanya biashara wake.

Mtume Muhammad alikubali na kuanza kufanya biashara na katika safari yake ya kwanza alifuatana na Maisara ambae alikuwa ni mtumwa wa bi Khadija.
Wakati Mtume Muhammad (S.A.W) aliporejea kutoka safari ya biashara, mapato yaliongezeka mara dufu na kumfanya Bi khadija kuzidi kuvutiwa nae. Sio hilo tu lakini hata Maisara mwenyewe alieleza utofauti aliokuwa nao Mtume Muhammad (S.A.W) ambapo alidiriki kununua vyakula vya bei rahisi ili asimtie hasara tajiri yake.
Pia katika sahihi bukhari (2262) imeelezwa kuwa Baada ya  bi khadija kuzielewa kwa undani tabia halisi na alivutiwa nae na alihisi wazi huyo ndiye aina ya Mume ambae alikuwa anamuhitaji katika maisha yake, kwani yeye tayari aliuwa mtu mzima aliye wahi kuolewa na kuzaa hivyo maisha ya ndoa alikua anayajua. Kwani wanaume wengi walitaka kumuoa lakini alikataa.

Alifanya haraka kumtuma rafiki yake Nafisa amueleze mtume (S.A.W)kuwa anataka afunge nae ndoa, nae alifanya haraka kwenda kumueleza.
Mtume (S.A.W) alikubali na alimtuma ami yake kwenda kutoa posa na haraka ndoa ikafungwa wa mahari ya Ngamia ishirini.alibahatika kuzaa nae watoto sita kati ya watoto saba.
Unapoelezea historia ya Mtume (S,A.W) huwezi kusahau tokeo la uarabati Al-kaaba ambapo kwa kipindi hicho mtume (S.A.W) alikuwa na umri wa miaka 35 ambapo kila kabila lilitaka kupata nafasi ya kujenga, baada ya mabishano ndipo likatoka wazo kuwa atakae ingia ndani kwa muda huo kutoka nje ndie atakae toa maamuzi ya nani abebe Jiwe jeusi.

Ghafla alitokea Mtume (S.A.W) na wote walimkubali atoe suluhisho nae aliamuru kila kabila litoe mtu mmoja kwa ajili ya kubela jiwe hilo. Ambapo alitandika kilemba chake na kila kabila kuchukua ncha moja na yeye akachukua ilobaki, na makabila yote yakawa yameshiriki katika ukarabati huo.(ibn hisham)

Pia katika sahihi Albuhari imeelezwa kuwa Wakati alipokaribia miaka 40 Ilikuwa ni desturi ya Mtume Muhammad (S.A.W) kujitenga kwa masaa adhaa akitafakari juu ya uumbaji wa Allah (SW), pia huko alikuwa akifanya ibada mbali mbali na kuchukia ibada za kushirikina.

Katika sehemu ziliuwa maarufu kutembelea ilikuwa ni Mlima nuur na pango la hira ambapo katika pangohilo ndipo alipopewa utume.
Pia katika kipindi hicho mtumw (s.a.w) alikuwa akipata ilham kwa kuota mambo ambayo yalikuwa yanatokea kweli. (Ibnu Hisham)
Wakati alipotimia umri wa miaka arubainikama ilivyo kawaida kwa mitume wengine Mtume Muhammad (S.A.W) aliabidhiwa juumu la kueneza nenola Allah (SW)kwa walimwengu wote. 

Na wahay wa kwanza kumshukia ulikuwa ni maneno matakatifu ya kuran. Wamekubaliana wana vyuoni kuwa siku halisi aliyo pewa utume mtume  Muhammad (S.A.W) ilikuwa ni siku ya jumatatu mwezi 21 ramadhan ambayo ni sawa na Agosti 10 mwaka 610 C.E.

Hapo ndipo zikashushwa aya tano za kwanza kwa mtume (S.A.W)ambazo zinatilia mkazo jambo la kutafuta elimu.
Hii ni kuonesha kuwa ni kwa iasi gani dini hii ya Uislamu inavyo thamini mwenye kujua mambo.na ndio maana Alla (SW) akawarahisishia pepo njia ya kwenda peponi wale wanao tafuta elimu.

Ukija katika maisha halisi ya jamii za sasa kuna baadhi ya watu kama kwamba hawajui kuwa kusoma ni amri.kiasi kwamba wanafikia hatua kuufanya udhaifu wao ni hoja ya kubishana juu ya jambo Fulani.

Mtu anafikia hatua ya kusema `hata kama sijasoma laini kwa hili hunidanganyi` msemo huu ni silaha ya wasiokubali kubadilika kwa kutojua lakini pia kutotaka kusoma.

Pia kuna  watu wanao soma upande mmoja wa elimu na kubeza upande mwengne wa elimu kwa kisingizio tu cha kuona upande huo hauna maana.

Muhadhiri wa Mkuu wa Kitivo cha Masomo ya uislamu kutoka Chuo Kikuu Cha Waislamu Cha Morogoro Abdi Kassim Jiba anaeleza kuwa kufanya hivyo ni uwelewa mbaya wa makusudo ya aya tano za kwanza zinazoonesha umuhmu na ulazma wa kusoma kwa waislamu , kwanii kur- ani imeeleza wazi namna mtu anavyotakiwa kuwa makini katka kuelewa dhana ya kusoma.

‘’hebu chukulia mfano mdogo tu wa teknolojia ya anga na masomo ya sayansi wakati kurani tukufu inashuka yalielezwa lakini swali la kujiuliza teknolojia ya karne ya saba na sasa ni sawa hayo yamekuja kwa kusoma’’ anaeleza Jiba.

Pia anaendelea kueleza kuwa kuisoma dini ni muhimu kwani bila ya kusoma hata ibada zitakuwa na mushkeli. Kwa mujibu wa jiba anaeleza Tatizo hilo linakuja kutokana na mfumo wa elimu hauwapi fursa wanafunzi wazazi na jamii kwa ujumla nafasi ya kusoma na kuelewa dhana ya ``soma kwa jna la mola wako aliiyeumba`` lakin kama llingejulikana hiya yote yasinge tokea.

Mkuu huyo anatoa suluhsho katika makala hii ambapo anasema ni kuwaandaa walimu ambao wataweza kuelimisha kizazi chote juu ya umuhimu wa elimu katika Nyanja zote za maisha , lakini jamii kutaka hasa kwa moyo mmoja kujua na kutekeleza yaliyomokatika elimu kivitendo.

Akitolea mifano mbali mbali mkuu huyo ameitaja aya ya pili akisema huwezi kujua kama binaadamu kaumbwa kwa tone la manii bila kufanya uchunguzi na uchunguz ni sayansi, kurani imeeleza kila kitu lakini huwezi kuelewa bila ya kuwa mdadisi na msomi.

 Na ndio maana mwanaadamu akaumbwa kuwa iongozi hapa duniani wa kuitawala dunia, lakini yote yanafanikiwa kwa kuelewa majukumu yote.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.