Habari za Punde

Haki Jamii kuzidisha kasi ya kutoa elimu juu ya madhara ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia

Na Salmin Juma, Pemba

Wanajumuia ya  “HAKI JAMII” inayojishuhulisha na kupinga matendo ya ukatili na udhalilishaji  wa kijinsia nchini iliyopo Wilaya ya Chake Chake wamesema kua wameamua kujipanga  vyema kupambana na matendo hayo  na kero mbalimbali zinazo zinazoikabili jamii ili kufanikisha makundi yanayonyanyaswa kuishi kwa furaha kama ilivyo kwa watu wengine.

Hayo yameelezwa na Msaidizi Mwenyekiti Bw Kombo Ali Khamis wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa Habari huko Ofsini kwake  Chanjamjawiri mkoa wa kusini pemba ambapo amesema vitendo vya udhalilishaji ni janga kubwa kwa taifa na kadiri ya siku zinavyosonga ndivyo vitendo hivyo vinaongezeka.

Akizungumzia katika mikakati waliyoipanga ili kukomesha matendo hayo amesema kua, kitu cha kwanza watazidisha kasi ya utoaji elimu kwa jamii juu ya madhara yatokanayo na matendo hayo.

“tumeanzia katika skuli mbalimbali, pia tunampango wa  kuelekea kwa  viongozi wa shehia kisha wanajamii wenyewe,tunaimani kua kasi hii itapunguza kiwango kikubwa cha matendo haya’ alisema Khamis.

Katika hatua nyengine M/kitu huyo  amefahamisha kua, wameshaanza hatua madhubuti za kupambana na  utumiaji wa madawa ya kulevya unaosababisha kuongezeka kwa matendo maovu yanayo fanywa na vijana wanaotumia madawa .

Amesema elimu ndio kitu cha msingi kwao,hivyo pia wameshaanza kuwatafuta watumiaji wa madawa hayo na kuwapatia elimu hukUwakiwaonyesha kiundani kabisa madhara yatakayoendelea kujitokeza iwapo kama hawatoachana na hali hiyo.

Mwisho kabisa ametoa wito kwa Serikali na mashirika binafsi na kila mdau wa hayo kushirikana kwa pamoja  kupiga na kutokomeza matendo machafu ya udhalilishaji kwani jamii inaendelea kuteseka na janga hilo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.