Habari za Punde

Shehia ya Shumba vyamboni waungiwa maji safi na salama majumbani

Na Salmin Juma, Pemba

Wananchi  wa  Gombe na Nguuni Shehia ya Shumba  Vyamboni wameshauriwa kuitumia fursa waliyoipata kwa kuunga huduma ya maji safi na salama katika majumba yao .

Ushauri huo umetolewa na Afisa Mdhamini  Wizara ya Ardhi Maji Nishati na Mazingira  Juma Bakar Alawi  wakati  alipokwa akikabidhi mipira ya maji ZAWA kwa wananchi wa shehia hiyo kwa mashirikiano ya Mamlaka ya maji  na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni  .
  
Amesema  wameweza kuwafikishia  wananchi  huduma hiyo ya maji  safi na salama ili kuwaondolea kero ambayo iliokuwa ikiwasumbua kwa muda mrefu  na kuwataka kuichangia huduma hiyo.

Nae Mkurugenzi wa ZAWA  Omar  Bakar Mshindo amesema kuwa ufungaji wa mita kwa wananchi wanaohitaji kuungiwa huduma ya maji ni jambo la lazima kwani  fedha  zinazochangiwa na wananchi  zinatumika kwa ajili ya manunuzi ya baadhi ya vifaa .

kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni Hamad Mbwana amesema upatikanaji wa mipira hiyo ya kusambazia huduma  ya  maji  kwa wananchi ni kupitia fedha za  mfuko wa Jimbo ambapo jumla ya maroli saba yenye thamani ya sh million saba yamenunuliwa .

Baadhi ya wananchi wa shehia hizo  wameishukuru serekali ya mapinduzi ya zanzibar kupitia wizara ya Ardhi maji na Nishati  kwa juhudi kubwa iliochukua ya kuwapelekea huduma ya maji safi na salama katika vijiji vyao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.