Mheshimiwa Riziki Pembe Juma
ambaye ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (Kushoto) akipokea Hati
za kukabidhiwa Chuo cha Sayansi za Afya
kutoka kwa Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo, Waziri wa Afya Zanzibar
Bwana
Iddi Haji Makame, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Utawala na Fedha (Kulia), akikabidhi
Hati za Chuo hicho kwa Mheshimiwa Riziki Pembe Juma kwa niaba ya Mheshimiwa
Dkt. Khalid Salum Mohamed, Waziri wa Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Riziki Pembe Juma,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar akikabidhi Hati za Taasisi
zilizounganishwa na SUZA kwa Mheshimiwa Said Bakari Jecha, Mwenyekiti wa Baraza
la Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
Mheshimiwa Rashid Ali Juma
(Kulia), Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo akikabidhi Hati za Taasisi
ya Maendeleo ya Utalii Zanzibar (ZIToD) kwa Mheshimiwa Riziki Pembe Juma. Katikati
ni Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar tarehe 16
Januari, 2017 ilikabidhiwa rasmi Chuo cha Utawala wa Fedha Zanzibar (ZIFA),
Chuo cha Sayansi za Afya (CHS), na Taasisi ya Maendeleo ya Utalii Zanzibar
(ZIToD) ambazo zote kwa pamoja sasa zinakuwa chini ya Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA).
Taasisi zilizounganishwa na SUZA zitaendesha shughuli zake kama kawaida lakini zikiwa na majina mengine ambapo
iliyokuwa ZIFA sasa itakuwa ni Skuli ya Biashara, CHS itakuwa chini ya Skuli ya
Afya na Sayansi za Tiba ambapo ZIToD itakuwa ni Taasisi ya Maendelo ya Utalii.
Makabidhiano hayo yalifanywa na Mheshimiwa Mahmoud
Thabit Kombo, Waziri wa Afya ambaye aliikabidhi CHS, Mheshimiwa Rashid Ali
Juma, Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo aliyeikabidhi ZIToD na
Mheshimiwa Dkt. Khalid Salum Mohamed, Waziri wa Fedha na Mipango ambaye
aliwakilishwa na Bwana Iddi Haji Makame, Kaimu Mkuu wa ZIFA.
Makabidhiano hayo yalifanyika kufuatia
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi mnamo tarehe 16 Oktoba, 2016 kuidhinisha
kuunganishwa kwa taasisi hizo kwa kusaini Sheria namba 7 ya mwaka 2016
iliyopitishwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar
na kufuta Sheria zilizoanzisha taasisi hizo. Aidha Sheria hiyo iliyosainiwa na
Dkt. Shein kuunganisha taasisi hizi imeifanyia marekebisho Sheria Namba 11 ya
mwaka 2009 ambayo nayo iliirekebisha Sheria Namba 8 ya 1999 ambayo ndio
ilianzisha Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar .
No comments:
Post a Comment