MKURUGENZI Idara ya Maendeleo ya Uvuvi Zanzibar Mussa
Aboud Jumbe, akielezea hatua wanazopaswa kufanya wajumbe wa Kamati tendaji ya
PECA, baada ya kuja kwa mradi mpya wa uhifadhi wa uvuvi SWIOfish, kwenye
mkutano uliofanyika ukumbi wa Makonyo Wawi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
WAJUMBE wa Kamati tendaji ya PECA, wakimsikiliza
Afisa Mdhamini Wizara ya mifugo na uvuvi Pemba, Mayasa Hamad Ali, wakati
akifungua mkutano wa kuwasilisha mradi wa usimamizi wa uvuvi SWIOfish,
uliofanyika ukumbi wa mikutano Makonyo Chakechake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
-Ni baada ya Pweza, dagaa, pono kuhifadhiwa
Na mwandishi maalum, Pemba
KILA mmoja ni shahidi kuwa serikali kupitia
wizara inayoshighulia uvuvi, imekuwa kiguu na njia kila uchao, kuhakikisha
sekta hiyo inaongeza pato la taifa.
Elewa kuwa, pato
la taifa hupanda baada ya wananchi au walengwa nao kunufaika kupitia sekta
husika, kwa mfano kwenye kilimo, wastani wa pato la taifa la
kila mtu limeongezeka na sasa na kufikia shilingi 1,552,000 sawa na dola za
Kimarekani 939 mwaka 2014.
Hapa
ni ongezeko kubwa, kutoka pato la shilingi 1,384,000 sawa na dola za Kimarekani
866 kwa mwaka 2013, ambapo taarifa zineleza kuwa sekta ya kilimo ikiwani pamoja
na uvuvi, imetajwa kuchangia.
Juhudi za serikali katika kunawirisha sekta ya
kilimo chini ya uvuvi, hazikuanza leo, maana kama unakumbu kumbu nzuri, basi
tulianzia kwenye mradi wa MACEMP, ambapo leo tena tunao wa SWIOFish.
Washirika wetu wa maendeleo wamekuwa nasi bega kwa bega kila
hatua na kila nyanja, na wakati mwengine tumekuwa tukifanikiwa kupata miradi
kadhaa, tena kutokana na matumizi sahihi ya fedha.
Leo tena Mashirika mawili makubwa kutoka Marekani yanayotoa
ufadhili wa miradi ya maendeleo ya GIF na IDA, yameshabisha hodi nchini kwetu
kwa ujio wa ‘Mradi wa usimamizi wa uvuvi
kusini Magharibi mwa bahari ya hindi’ au kwa ufupi SWIOFish.
Mradi huu, kwa hatua za awali za utekelezaji, umetia nanga
kwenye nchi tatu za Mozambique, Comoro na sisi hapa Tanzania hadi visiwa vyenye
samaki wengi vya Zanzibar.
SWIOFish, sasa unakuja kuendeleza mema yalioachwa au kufikiwa na
mradi wa MACEMP, ambapo maradi huu sasa unalenga zaidi kukuza pato kwenye sekta
ya uvui.
Lengo baada ya kuwanufaisha wavuvu, nao uchumi wa Zanzibar
kupitia mradi huo ambao kwanza utatelekezwa kwa miaka sita, utapaa zaidi.
Maana aliekuwa waziri wa fedha wa Zanzibar, Omar Yussuf Mzee,
anasema kimuundo, uchumi wetu umeendelea kuchangiwa zaidi na sekta ya huduma ikifuatiwa
na kilimo.
Alitoa mfano kuwa, mwaka 2014, sekta ya huduma ilichangia
asilimia 44.7, ikionesha kupanda kwa mchango wake kutoka asilimia 41.5 wa mwaka
2013
Hali hii imetokana na kuimarika kwa sekta ndogo za habari na
Mawasiliano, fedha, taaluma, ufundi na sayansi, mchango wa sekta ya kilimo kwa
mwaka 2014, umepungua na kufikia asilimia 27.9 kutoka asilimia 30.4,
mwaka 2013 kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa mpunga na mazao mengine ya
chakula na kupungua kwa uzalishaji wa mazao ya biashara, hasa karafuu.
Sasa ujio wa
mradi huo uliochini ya Mratibu wake wanadada Ramla Talib Omar kwa hapa Visiwani,
unakuja kuwahifadhi samaki aina tatu kuu kwa kuanzia.
Aina moja
ambao mradi huu wa SWIOFish unalenga, ni wale samaki wanaoishi kwenye
matumbawe, ambayo ni aina fulani ya mawe yenye bustani, ambapo tunasema ni
nyumba ya samaki.
Hapo
watakaohifadhiwa atakuwemo, kolekole, pono, changu, kundaji, ambapo hili
halitofanywa kwa kukurupuka, bali wale waliohifadhi eneo la mkondo wa Pemba
PECCA, ndio watakaoifanya kazi hii ya kuibua maeno husika.
“Kwa Pemba
nyinyi wajumbe wa PECCA, ndio ambao mtakaa na wavuvi wenu, kisha mtueleze eneo
gani mnadhani kuna samaki wengi wa matumbawe, ili mradi huu utie nanga’’, alisema
Mratibu wa mradi huo Ramla.
Aina
nyengine ambapo mradi huu wa SWIOFish unalenga kuwahifadhi, niwale samaki aina ya pweza na ngisi, ambapo kila
mmoja ni shahidi kwamba wameanza kupungua.
Hili
lilielezwa vyema na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi Zanzibar Mussa
Aboud Jumbe, kwamba ni maeneo machache sana yenye nyumba za pweza.
“Mnapo kwenda
kuibua maeneo yenye kuishi hasa pweza, angalie sana kwenye miamba, maana pweza
haishi mchangani, lazima makae vyema na wavuvi’’,alibainisha.
Kwenye
mkutano wa siku moja wa kuwasilisha mradi huo, mbele ya wajumbe wa kamati
tendaji wa PECCA uliofanyika Chakechake Pemba, wajumbe hao walionekana
kufarajika.
Katibu wa
PECCA Khamis Sharif, yeye anasema kama mradi huo utatekelezwa vyema kwa mujibu
wa maandiko yalivyo, basi manufaa yataonekana.
“Mimi sasa
nimeelewa nini mradi wa SWIOFish unakuja kufanya nini kwa wavuvi, kilichobakia
ni kuhakikisha unatekelezwa kama ulivyo, ili manufaa yaonekane’’,aliweza wazi.
Lakini pia
mradi huo mpya ambao kwa Zanzibar umeshatengewa dola za Marekani milioni 11,520,000
sawa na asilimia 40 ya fedha zilizoingizwa Tanzania, pia unangalia uhifadhi
samaki ya jamii ya dagaa (samaki wanaoeleya).
Hapa
anaingia dagaa mono, bakari kichwa, dagaa manyama na kaka yao kibua na kama
kuna wengine wale wanaoelea, naamini baada ya miaka sita (6) ya hatua ya kwanza
ya utekelezaji manufaa yataonekana.
Kama ni mtu
wa kumbu kumbu, hata mradi wa MACEMP ambao sasa hatunao tena, ilifanya shughuli
za utafiti wa viumbe wa bahari kama vile kamba, kaa, jodari, samaki wa maji ya
kuelea, lakini matokeo yake hayajafikia, katika kiwango kilichotarajiwa, sasa
SWIOFish ndio muarubani wa hilo.
SWIOFish,
kama ulivyonisoma hapo juu, kwa hatua hii ya kwanza utatia nanga nchini Tanzania
(hadi Zanzibar), Mozambique and visiwa vya Comoro, ambapo hatua nyengine
itaanza baada ya miaka sita.
Pamoja na
kazi hiyo, lakini pia SWIOFish unamalengo mengine ya kukuza usimamizi makini wa
kuzipa vipaumbele vya shughuli za uvuvi kwa ngazi ya Kanda, Kitaifa na
Kijamii
Tunaposema
kikanda kwenye mpangu huu, ni baadhi ya nchi zitajiunga na SWIO moja kwa moja,
tangu unapoanza kama Tanzania ambapo nchi nyengine zitajiunga baadae kwa mujibu
wa taratibu.
Kwenye ngazi
ya kitaifa, mipango ya usimamizi wa shghuli za uvuvi ambayo imepewa
kipaumbele itatekelezwa, ili manufaa ya kweli na endelevu yaonekane.
Yapo maeneo
mengine kama ya kijamii, ambapo hasa lengo lake ni kuongezeka kwa Kamati za usimamizi
kwa angalau asilimia mbili (2), hukunao walengwa sasa kuongezeka kwa Idadi ya
watakaofaidika moja kwa moja.
Mradi huu wa
usimamizi wa uvuvi kusini magharibi ya bahari ya hindi, SWIOFish, sheria ya
Uvuvi no 7 ya mwaka 2010 itafanyiwa mapitio, sambamba na uanzishaji wa na
uimarisha wa mfumo wa taarifa za takwimu zitokanazo na, mbinu, leseni,
usafirishaji na mapato.
Lakini kuna
maeneo teule katika mpango huu yatasaidiwa kama vile ujenzi wa kituo
cha utafiti na ofisi mpya ya eneo la hifadhi mbili mpya za Hifadhi ya
ghuba ya Tumbatu ‘TUMCA’ na hifadhi ya Bawe ‘CHABAMCA’.
Kwa Unguja
mradi huu utatekelezwa kwenye eneo la hifadhi ya Menei ‘MENAI’ na eneo la
hifadhi ya Mnemba MNEMBA, ambapo kwa Tanzania (Zanzibar) wao wataendelea na
mpango kwa miaka 15 utakapokamilika hatua kwa hatua.
Mwenyekiti
wa wavuvi wa wilaya ya Micheweni Mkubwa Said Ali, anaona mradi huu unaweza
kuzaa matunda kutokana kuwa na lengo la uhifadhi wa samaki.
“Mimi
nimeshaanza sasa kuhifadhi kwenye bahari ya Makangale, sasa naamini kama mradi
huu utaingia kwenye eneo langu basi uvunaji wa samaki utaongezeka’’, alisema.
Sheihan
Mohamed Sheihan ambae ni Mwenyekiti wa wavuvi wilaya ya Mkoani, amewataka
wavuvi kushirikiana katika hilo ili kuona lengo la mpango huo linafanikiwa.
Kombo Hamada
Juma wa Chakechake ambae ni mvuvi anasema kwa hatua za maandishi mradi
unaonekena kuja na jambo jipya na hasa ikiwa utatekelezwa ipasavyo.
“Mbona mradi
huu wa SWIOFish, una nia nzuri kwa wavuvi na wananchi wote, maana unapogusa
kuhifadhi samaki neema kwa kila mmoja’’,alifafanua.
Khamis Haji
Mohamed wa Wambaa, yeye aliomba suala la elimu lipewe kipaumbele kwa walengwa,
ili kuepusha majaribu ya migogor baina yao na watendaji wa PECCA.
Kila mvuvi
sasa baada ya kupata taarifa hizo, yuko macho kuangalia mradi huu mkubwa ambao
unatazamiwa kuwakomboa wavuvi.
No comments:
Post a Comment