KARANI wa Upigaji wa Kura katika kituo cha skuli ya
Wesha Wilaya ya Chake Chake, akimpatia karatasi ya Upigaji wa kura ya Udiwani
wadi ya Ndgoni mmoja wa wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MMOJA wa Akinamama wa shehia ya Ndangoni Wilaya ya
Chake Chake, akipiga kura katika kituo cha Skuli ya Wesha, katika uchaguzi wa
Udiwani wa wadi ya Ndagoni.(PICHA NA
ABDI SULEIMAN, PEMBA).
WANANCHI wa wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake,
wakiangalia majina yao katika kituo cha Skuli ya Wesha, kabla ya kupiga kura ya
kuchagua diwani wanayemtaka katika uchaguzi mdogo wa udiwani wadi hiyo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
KARNI wa wapiga kura katika kituo cha Skuli ya
Wesha, akihakiki majina ya wapiga kura katika karatasi maalumu ya Tume ya
Uchaguzi Zanzibar, kabla ya Mtu kupiga kura huko katika skuli ya Wesha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MAKARANI wa tume ya uchaguzi Ofisi ya Pemba,
wakijaza majina ya wananchi baada ya kuhakikiwa jina lake katika karatasi ya
kupigia kura, katika kituo cha kupigia kura Skuli ya Wesha, katika uchaguzi
mdogo wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA
NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MMOJA ya wananchi akitumbukiza kura yake katika
sanduku maalumu, baada ya kupiga kura kumchagua diwani anayemtaka, katika
uchaguzi mdogo wa wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Mhe:Jecha
Salum Jecha akikagua maendeleo ya Upigaji wa Kura za uchaguzi mdogo Wadi ya
Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA
ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MGOMBEA wa Udiwani wadi ya Ndagoni kupitia Chama cha
Mapinduzi CCM, Arafa Kassim Abass akihakikiwa jina lake na mmoja kati ya
makarani wa Uchaguzi katika kituo cha skuli ya Ndagoni kabla ya kwenda kupiga
kura.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MGOMBEA wa Udiwani wadi ya Ndagoni Kupitia Chama cha
Mapinduzi CCM, Arafa Kassim Abass akitumukiza karatasi yake ya kupigia kura
katika sanduku maalumu la Uchaguzi katika wadi ya ndagoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MGOMBEA udiwani wadi ya Ndagoni kupitia chama cha
ADC, Khamis Juma Abdalla akipiga kura katika uchaguzi mdogo wa wadi ya Ndagoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MWAKILISHI wa Jimbo la Ziwani Suleiman Makame Ali
(mwenye suti) akizungumza na mgombea Udiwani wadi ya Ndagoni kupitia chama cha
ADC, Khamis Juma Abdalla katika kituo cha kupigia kura skuli ya Wesha Wilaya ya
Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN,
PEMBA).
No comments:
Post a Comment