Habari za Punde

Uchaguzi wa Diwani wadi ya Ndagoni, Chakechake Pemba

 KARANI wa Upigaji wa Kura katika kituo cha skuli ya Wesha Wilaya ya Chake Chake, akimpatia karatasi ya Upigaji wa kura ya Udiwani wadi ya Ndgoni mmoja wa wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 MMOJA wa Akinamama wa shehia ya Ndangoni Wilaya ya Chake Chake, akipiga kura katika kituo cha Skuli ya Wesha, katika uchaguzi wa Udiwani wa wadi ya Ndagoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 WANANCHI wa wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake, wakiangalia majina yao katika kituo cha Skuli ya Wesha, kabla ya kupiga kura ya kuchagua diwani wanayemtaka katika uchaguzi mdogo wa udiwani wadi hiyo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 KARNI wa wapiga kura katika kituo cha Skuli ya Wesha, akihakiki majina ya wapiga kura katika karatasi maalumu ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar, kabla ya Mtu kupiga kura huko katika skuli ya Wesha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 MAKARANI wa tume ya uchaguzi Ofisi ya Pemba, wakijaza majina ya wananchi baada ya kuhakikiwa jina lake katika karatasi ya kupigia kura, katika kituo cha kupigia kura Skuli ya Wesha, katika uchaguzi mdogo wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 MMOJA ya wananchi akitumbukiza kura yake katika sanduku maalumu, baada ya kupiga kura kumchagua diwani anayemtaka, katika uchaguzi mdogo wa wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Mhe:Jecha Salum Jecha akikagua maendeleo ya Upigaji wa Kura za uchaguzi mdogo Wadi ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).

 MGOMBEA wa Udiwani wadi ya Ndagoni kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Arafa Kassim Abass akihakikiwa jina lake na mmoja kati ya makarani wa Uchaguzi katika kituo cha skuli ya Ndagoni kabla ya kwenda kupiga kura.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).

 MGOMBEA wa Udiwani wadi ya Ndagoni Kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Arafa Kassim Abass akitumukiza karatasi yake ya kupigia kura katika sanduku maalumu la Uchaguzi katika wadi ya ndagoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
 MGOMBEA udiwani wadi ya Ndagoni kupitia chama cha ADC, Khamis Juma Abdalla akipiga kura katika uchaguzi mdogo wa wadi ya Ndagoni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).
MWAKILISHI wa Jimbo la Ziwani Suleiman Makame Ali (mwenye suti) akizungumza na mgombea Udiwani wadi ya Ndagoni kupitia chama cha ADC, Khamis Juma Abdalla katika kituo cha kupigia kura skuli ya Wesha Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.