Wakiri TAMWA kupitia WEZA II, imewapa
mwarubanini wa maisha yao
NA HAJI NASSOR, PEMBA
“Hee…kumbe hata ukili wafanywa
kipochi na mkoba wa lap top, sisi kwenye ushirika wetu hili ni jambo jipya
sana…..tuliozea ile mikoba ya zamani tu’’,ndio kauli ya Tamima Salum Ali wa
Kengaja.
Mama
huyu anatokea kwenye ushirika wa ‘Hatima njema’ unoajishughulisha na ususi wa mikoba
inayotumia rasilimali ya ukindu, amewawakilisha wenzake kwenye mafunzo ya
mikoba ya kisasa.
Tamina
anamini sasa, kwa aina mpya na ya kisasa ya mikoba wanayofunzwa na TAMWA
kupitia WEZA II, sasa mwanga wa maisha yao kupitia ushirika wao yanakaribia.
“Kwa
muda mrefu sisi tuliganda kwenye kutengeza aina moja pekee, ambayo ina umbo la
bao, lakini sasa jinsi ukili ulivyosarifiwa hatuna shaka maisha kupitia ushirika
wetu yataimarika’’,anasema.
Akiwa
kwenye mafunzo yaliofanyika Kiuyu kwa muda wa siku tatu, kwa makundi tofauti
anasema kumbe, Tamima kama TAMWA kupitia WEZA II, wengepata mradi mapema na
kuwapa mafunzo hayo, leo wengekuwa kwenye hadhi nyengine.
Tamima
anaamini sana mafunzo ya kutengeza mikoba ya kisasa, hana wasiwasi wa soko kama
ilivyokuwa kwa mikoba waliokuwa wakitengeza wao, bila ya kupata utaalamu.

Lengo
la mfunzo hayo kwa mujibu wa Mratib wa mradi huo wa WEZA II, ni kuona wanawake
wanaondokana na umaskini lakini kupitia umoja wao waliojikusanya kwenye vikundi
vya ushirika.
Ndio
maana kwa ari na moyo wa TAMWA kupitia WEZA II, ilikaa meza moja na wafadhili
wao Milele Foundetion na kupatiwa mradi huo wa miaka mitatu.
WEZA
ni mradi wa kuwawezesha wanawake kicuhumi ambao kwa mara ya kwanaza uliingia
kisiwani Pemba mwaka 2008, ukiratibiwa na Chama cha Waandishi wa habarai
wanawake Tanzania TAMWA ofisi ya Zanzibar.

Sio
tu kutoa mafunzo pekee, bali hata baadae vipo vikundi vya ushirika ambavyo
vitabahatika kununuliwa cherehani maalumu, ili kuiremba na kuipendezesha vyema
mikoba hiyo ya kisasa wanayofundishwa.
“Wapo
wanawake kwenye vikundi vya ususi wa mikoba, watapatiwa wameshapatiwa mafunzo,
lakini hata wale wanajishughulisha na upandaji w amboga mboga, nao TAMWA
imewaona’’,anasema.
Maulid
Saleh Hamad, nae kupitia kikundi chao cha ushirika kinachoitwa ;Nguvu Yetu
Umoja Wetu’ Kiuyu wilaya ya Wete, yeye anasema wala ndani ya ushirika wao,
hawakua na habari kwamba ukili unasarifiwa.
“Sisi
ilikuwa tukisuka mikoba na kisha inakaa bila ya kupata soko, maana hatukuwa na
aina mpya ya kumvutia mteja, lakini sasa TAMWA imeshatuma njia ya kujikomboa’’,anasema
Maulid.
Yeye kwa upande wake anasema anachongoja ni kumalizika kwa mafunzo hayo ili nae awaelekeze
wenzake tisa (9) ambao hawakupata bahati ya kuhudhuria mafunzo hayo adhimu na
admimu.
Hata
mwanaushirika kutoka “Tupande’ kilichopo Kiungoni Kimango Mfaunda Faki Hamad
anasema tangu walipoanzisha ushirika mwaka 2012, hawajahi kupata mafunzo ambayo
yanatoa mwanga wa maisha kama hayo.
Anaona
sasa, kupitia mafunzo hasa kwenye ushirika wao, ni kukaza kamba ili kushona
mikoba ya kileo, ambayo imekuwa ikipendwa sana na watu mbali mbali wakiwemo
watalii.

Mbinu
wanayoitumia ili kusaka soko, sio kubwete nyumbani bali wamekuwa wakigawanana
majukumu, ili kuhakikisha mwisho wa siku wanafikia malengo yao.
Ndio
maana mkufunzi na mjasiriamali wa mafunzo hayo alieaminiwa na TAMWA, Nassra
Salum Mohamed wa Kiuyu, anasema suala la soko kwa wanaushirika sio kukaa
nyumbani na kulilia bali inawapasa kuchakarika.
Kwa
uzoefu wake, anasema lazima kwa siku za awali wanaushirika wajitutumue kutoka
wanakoishi na kwenda hata maofisini au sehemu wanazofikia watalii au mkusnyiko
wa watu.
Maana
anasema hadi mkoba huo wa kisasa kukamilika kwa zana zake, zote wastani katia
ya shilingi 15,000 hadi shilingi 17,000 hutumika, ingawa kwa bei ya kawaida
mkoba huo kisha huuzwa kati ya shilingi 22,000 hadi shilingi 25,000.
Ingawa
katika kuukamilisha mkoba huo wa kisasa, lazima uwe na ukindu na kisha
kuupakasa, kisha kupikwa kwa rangi moja au mbili, na kuushokana kama kawaida
kwa kutumia utembo au nyuzi za kipolo.
Baadae
hulazimika kuwa na kipolo ambacho huunganishwa na ukili huo, ambao huzibwa kwa
kitambaa, kabla ya kuweka zipu ndogo na kubwa, kutokana na aina ya mkoba
unaohitajika.
Hili
lilimshangaaza na kumpa matumaini makubwa, Khadija Ramadhan Ali anaetokea
ushirika wa “Tupendane group’ kwamba mafunzo hayo, anaamini ni mazuri maana
sasa ukili wa mikoba watauviringa wapendavyo.
“Mimi
mafunzo nayona mazuri sana, na natamani yasimalize, maana sijaonapo kuwa hata
kipochi na mkoba wa kumputa waweza kufanya, hapa lazima soko
litapatina’’,anasilimulia.
Kwake
yeye anasema ndani ya ushirika wao kama waliopoteza muda kuchelewa kupewa
mafunzo hayo, ambayo anaona sasa kama mkombozi ndani ya ushirika wao.
Aliwaomba
TAMWA kupitia WEZA II, kuharakisha kuwapatia mashine au sherehani za kushonea
mikoba hiyo, maana kwa kutimia cherhani za kawaida kazi haiendi vyema.
Asha
Makame Alawi nae alijikuta ndani ya mafunzi hayo, ya utengezaji wa mikoba,
vipochi na mikoba maalum ya ofisini kwa kutumia ukindu, akiwawakilisha wenzake
wa ushirika wa ‘Yarabi tupe’.
Anasema
kabla ya ujio wa TAMWA kupitia WEZA II, hawa kuwa wakijua namna ya ushoni wa
mikoba hiyo, ambayo anasema kumbe walichelewa sana kupata mafanikio.
“Hii
mikoba ni aina mpya, maana ukiwa mbali utafikiri ni ile ya madukani inayotoka
Ulaya na Arabuni, lakini kumbe ni ukindu uliosarifiwa’’,anasema.
Hakuwa
tofauti na mjasriamali Salha Hilali wa Chakechake kijiji cha Mvungwa, ambae nae
kabla ya mafunzo hayo, hakuwa akielewa lolote jinsi ya ususi wa mikoba hiyo.
“Mimi
naishukuru sanaTAMWA na wafadhili wake Milele Foundation kwa kutuona kwenye
ushirika wetu, maana ilikuwa hii mkoba twaiona kwenye tv, lakini leo
nshfundishwa na najua kutengeza sasa’’,anafafanua.
Msimamizi
wa Mradi huo wa kisiwani Pemba Jit-hada Abdalla Salim yeye anasema kama
wanawake hao 50 watawafunza wenzao, basi elimu hiyo ya utengenezaji wa mikoba
ya kisasa itaenea.
“Lengo
hasa sio hawa wanawake walio kwenye vikundi vya ushirika pekee, bali kila
mwanamke wa kisiwa cha Pemba, apate mafunzo haya kupitia
walioshiriki’’,anafafanua.
Ndio
maana amekuwa wakiwataka mara kwa mara kuhakikisha wanafuatilia kwa kina
mafunzo hayo, ili wawe na uhakika wa kuwapa taaluma hiyo wenzao mbali mbali.
Lakini
hata Magrate Antony nae kutoka Kikwajuni Unguja ambae alikuwa mmoja kati ya wakufunzi
ndani ya mafunzo, hayo alisema kama wakielewa vyema wanawake jinsi ya ususi wa
mikoba hiyo, wala hawatolalamikia soko.
“Mikoba
ya kisasa ya ukindu ambayo huwa na zipu na mfunikio kama ile kutoka nje,
hupendwa na wazawa na hata watalii, sasa lazima wanawake hawa wajipange ili
wavune matunda’’,anafafanua.
TAMWA
ilishawahi kuwapa mafunzo ya ususi wa mikoba, kilimo cha mboga mboga na jinsi
ya kusaka masoko, kupitia WEZA I ingawa kwa sasa imekuja na aina mpya ya
utengenezaji mikoba.
Kwa
wakati huo, wanawake waliyatambua masoko ya kuuzia bidhaa za mboga mboga na
mikoba, na sasa TAMWA kupitia WEZA II imetia nanga tena kisiwani Pemba ili
kuendeleza pale palipoaachwa na WEZA I.
Baadhi
ya wanaume waliozungumza na ukurasa huu, wanasema sasa wanawake ndio wanaojenga
familia kutokana na kuingia kwenye vikundi vya ushirika na kujipatia kipato.
Ali
Juma Ali ambae mke wake yumo kwenye ushirika wa ‘Umoja Wete Nguvu Yetu’ cha
Kiuyu anasema yeye sasa anakula matunda yanayotokana na jitihada za mke wake
kujiingiza kwenye ushirika.
“Lazima
wanaume sasa tuamke, maana wanawake wamekubali kujikusanya na kuweka anasa na
mambo mengine pembeni maana wameshajua umuhimu wa wao kuzisaidia
familia’’,alieleza.
Kombo
Hija Makame wa Mchanga mdogo anawashauri wanawake wenyewe kusimama kidete ili
kuhakikisha wanawekewa banki maalum, ili wapatiwe mikopo yenye masharti nafuu.
Hassan
Chumu Hassan wa Kwale yeye anasema, uhuru walionao wanawake kwa waume zao,
lazima wautumie vyema ili iwe chanzo cha kufika watakako.
Wizara
inayosimamia wanawake na watoto, imekuwa na mpango maalumu wa kuwawezsha
wananchi kiuchumi ambapo inalenga kuinua hali za wananchi kiuchumi.
Lengo
hasa ni kuwapatia wananchi hao wakiwemo wanawake, mikopo na kuwajengea uwezo wa
kiujasiriamali na kuwangunanisha katika vyma vya ushirika.
Kwa
2015/2016 pekee mikopo 337 kwa Unguja na Pemba ilitolewa kupitia Mfuko wa
Uwezeshaji wananchi kiuchumi, ambapo yakiwa na thamani ya zaidi ya shilingi
milioni 523 iliwanufaisha wananchi 1,907 wakiwemo wanawake 1,136 ndani ya
shehia 161 za Zanzibar.
Mwanaharakati
wa masuala ya wanawake Pemba, Stara Khamis Salim anasema lazima taasisi
zinazotoa mikopo zilegeze masharti hasa kwa wanawake, ili wakidhi vigezo na kuiomba.
Kwani
anasema “wanawake wamekuwa wakipewa mafunzo mbali mbali mfano kupitia wizara
husika na asasi za kiraia kama TAMWA, lakini hushindwa kuchukua
mikopo”,alieleza.
Mkuu
wa Mkoa wa Kusini Pemba Mwanajuma Majid Abdalla, akizungumza na wanawake kwenye
siku ya wanawake duniani ambapo kwa Pemba, ilifanyika Chakechake, alisema
lazima wanawake weke chonjo siasa wafanye kazi.
“Vikundi
vya ushirika endeleeni kujikusanya pamoja, ili muwe na sauti moja na hata iwe
rahisi kuomba mikopo ambayo ipo na haina masharti magumu’’,anasema.
Naibu
Katibu Mkuu wizara ya wanawake na watoto Zanzibar Mauwa Makame Rajaba,
anawashauri wanawake kutoshindwa kutekeleza shughuli zao kwa ukosefu wa mitaji,
maana sasa serikali imeshajipanga.
“Kama
kuna wanawake wanahitajia mashine kwa ajili ya kuendeleza shuguli zao, waandike
barua wizarani na kima cha fedha cha kununulia mashine husika, ili wapatie
fedha za mkopo zenye masharti wanayoyaweza’’,anafafanua.
Akizungumza
kwenye kipindi cha meza huur Evamarie Semakafu kutoka asasi ya Ulingo Tanzania
bara, anasema wanawake kama hawakusimama wenyewe katika kujikomboa kiuchumi,
inaweza kuwa ndoto.
Mwanaharakati
wa masuala ya wanawake Pemba, Jitihada Abdalla Salum, anasema mafunzo
yanayotolewa na TAMWA kupitia WEZA II, kama wanawake hao wakiyafahamu vyema,
yanaweza kuwa mkombozi.
Shemsa
Hakim Khamis dereva wa gari ya kuchukulia wageni (TAX) uwanja wa ndege wa
Pemba, anasema huu sio wakati wa wanawake kujibakiza nyumbani wakidhani
wanaweza kumalizia shida zao kila kitu.
“Wanawake
hasa walioolewa, wakiwa na dhana kuwa hata mchango wa harusi umsubiri muume,
ujue bado umelala usingizi mzito, hii ni karne ya mwanamke
kujitegemea’’,ameshauri.
Sheikh Massoud Hamad Ali wa Chakechake Pemba,
anasema dini ya kiislamu wala haijamkataza mwanamke kufanya kazi, cha
kuzingatia ni yenye heshima kama ujasiriamali.
No comments:
Post a Comment