Habari za Punde

Bi Shemsa Hakim: Dereva wa teksi anaeimudu kazi yake


 Bi Shemsa Hakim akisimama mbele ya gari yake ta Teksi

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.

Mwandishi Abdi Suleiman
“KWA sasa huna vya kuniambaia juu kazi yangu hii!!!!!!!!! kwangu ni kama kazi nyengine, nimekuwa nikipokea simu za wageni wanaohitaji huduma yangu wakiwa Dar au Unguja ndio kwanza wanapanda ndege” aliniambia Shemsa huku akitabasamu.

Mcheshi na mchangamfu kwa kila mtu wakati wote utakapomuona, ni dereva anayetulia wakati anapokuwa amepakiwa wateja na kuwapeleka sehemu wanazohitaji kwenda.

Shemsa Hakim Khamis (40), si mrefu wala mfupi ni mtu wa wastani, mwenye uso mpana wenye kungaraa kutokana na weupe wake, mchangamfu muda wote ikimtazama mara anacheka na kuinamia chini.

Mwishoni mwa mwaka 2016 alianza kazi ya udereva Taxi katika kituo cha Uwanja wa Ndege wa Karume Pemba, bila ya kujali yeye ni jinsia gani na kazi hiyo ikiwa imezoeleka kufanywa na wanaume.

“Kazi hii ni kazi kama kazi nyengine ikishakuwa umejiamini kuifanya na bila ya kujali maneno maneno ya watu, basi utafanikiwa chamsingi ni heshima inahitajika katika kazi hiii” alieleza Shemsa.

Bila ya kushawishiwa aliamua kujiingiza katika kazi hii ya Udereva wa Taxi katika uwanjani wa Ndege, kwa lengo la kujiajiri mwenyewe na kuacha utegemezi wa mume nyumbani.

Kwa sasa Shemsa ameanza kujizoelea wateja kutoka sehemu mbali mbali zaidi wanawake wenzake wanaofika Kisiwani Pemba, kulazimika kuhitaji huduma ya usafiri kutoka kwake.

Mzaliwa wa Chanjamjawiri mwaka 1977, alimaliza darasa la 10 mwaka 1989 katika skuli ya Chanjamjawiri, baada ya wazee wake kutengana alishindwa kupata nafasi ya kuendelea na masomo.

Anasema alilazimika kukaa nyumbani kumuhudumia mama yake, ambae kwa wakati huo tayari umri ulishamchukuwa, hali iliyofanya ndoto zake za kuwa rubani wa ndege kuanza kupotea na kuingia katika biashara ndogo ndogo.

“Nililazimika kupika Uji, Maandazi, vileja na biadhaa nyengine ndogo ndogo ili tuweze kupata pesa za matumizi, muda ukafika nikapata mume akaniona” alisema.

Mwaka 1995 niliolewa ambapo hadi sasa sikubahatika kupata mtoto, tunapendana sana mimi na mume wangu, yeye ni mfanya biashara na mimi ni dereva Tax tunasaidiana maisha.

Udereva Tax ulikuja baada kuwa na usafiri wangu binafsi, mwanzo nilimpa mtu kuendesha lakini maslahi yalikuwa magumu kupatikana nimeamua kuendesha mwenyewe na sasa nimejuwa faida zake, Changamoto zake.

Pia alimpa mtu kumuendeshea na kutokuona maslahi yoyote, kulazimika kuuchukuwa mwenyewe na kujuwa kama kuna faida au laaa, aliweza kushirikiana na mumewe na kuelewana.

“Mafunzo haya ya udereva nimeyapata kutoka kwa shemegi yangu hapa chake chake, alikuwa jioni jioni akinifundisha gari, nimefuata taratibu zote katika upataji wa leseni na sasa naweza kuendesha gari na kupeleka abiria sehemu yoyote ile” alisema.

Tokea kuingia katika kazi hii sijapata na matatizo yoyote, madereva wenzakengu wamekuwa wakinisaidia kwa kiasi kikubwa, kunipa mbinu za kupata wateja licha ya kuwa kuna zamu zake hapa, lakini ikifika zamu yangu wanazungumza na abiria na kuniambia nimpeleke sehemu fulani na nauli yake kiasi fulani basi.

Tokea kuwepo hapa lakini bado sijawahi kupata abiria mzungu au mgeni anayehitaji kwenda makangale, zaidi ni wa hapahapa mjini akitokea nitampeleka.

“Tayari wanawake wenzangu wameweza kufurahia na wako tayari kuungana na mimi katika kazi ya udereva wa Tax, hapa chamsingi heshima na nidhamu ndio kitu muhimu katika kazi hizii, usafi wa gari na dereva mwenyewe” alisema.

Kuhusu masuala ya Familia Shemsa anasema, Mumewe akiwepo hulazimika kwenda kazini mchana asubuhi huwepo nyumbani, kwa ajili ya kushughulikia mambo ya familia, akiwa hayupo hulazimika kwenda kazini asubuhi ili kuwahi namba kama walivyo wengine” alisema.

Mitazamo iliyopo mimi naichukulia kama hali ya kawaida tu, kazi ni kazi tu pesa ikiwa inapatikana, kuhusu abiria wasiokuwa na nidhamu, anasema ni heshima ya mtu, ambapo kwa sasa anajifundisha lugha ya Kiengereza kidogo kidogo.

Changamoto anazokumbana nazo, baadhi ya abiria wanapowakodisha gari kwa siku nzima, wengine kutokuwalipa pesa zao wapo wanaowalipa na wengine sio waaminifu na kazi.

Shemsa anasema biashara inavipindi, vipo vipindi biashara inakuwa nzuri na vipo vipindi biashara inakuwa mbaya, hata pesa ya mafuta ulioweka kwa siku ile huipati lakini ndio biashara.

Akifafanua malengo yake anasema ni kununua gari nyengine na kuwa na gari mbili, huku akiwataka wanawake wenzake kujitokeza kumuunga mkono katika fani hiyo.

Mdhamini wa kamisheni ya Utalii Pemba, Suleiman Amour Suleiman, anasema sekta ya Utalii Pemba inazidi kuimarika baada ya kujitokeza kwa dereva Tax Mwanamke.

Uwepo wa Shemsa katika Tax imefikisha madereva Tax 44 wanaume 43 na Mwanamke mmoja, ambapo sera ya Utalii kwa wote imeanza kutekelezwa kwa vitendo.

Anasema Shemsa ataweza kuwa ni moja ya chanzo kikubwa cha kushajihisha wanawake kuona kwamba kazi ya Tax ni sawa na kazi nyengine.

Mdhamini anasema wakati umefika wa kuona mabadiliko katika sekta ya Utalii, hasa kwa madereva Tax wanaochukuwa wageni katika sehemu mbali mbali za Kisiwa Cha Pemba kuwepo akinamama.

“Kazi ni kazi tu ikishekuwa ni yahalali basi hupaswi kuchagua kazi, Wengi sasa wanamtizama Shemsa atamudu kazi hii, ili na wawo waweze kuingia na kuanza kuchukuwa abiria” alisema.

Nifaraja sasa kuona lile lengo la serikali la utalii kwa wote limeanza kutoa matunda, kushiriki kwa wanawake dereva Tax kupeleka wageni, ikiwa utalii unatoa ajira sasa imeanza ya kuendesha magari na kupeleka wageni, sekta ya utalii imepiga hatua pemba.

Aidha alimtaka Shemsa kutokuvunjika moyo na kunufaika na keki ya sekta ya utalii, kujitahidi kuwa nadhifu ili kuweza kupata abiria kwa wingi na kuongeza pato lake.

Mdhamini wa Magari ya Kukodishwa Mkoa wa kusini Pemba, ambaye pia ni dereva wa Tax Abdalla Ali Abdalla, alisema PESTA wamefurahia sana kuona sasa Pemba inadereva TAX mwanamke katika Uwanja wa Ndege.

Uwepo wake wamepiga hatua na ndio dereva wa kwanza kwa Pemba Tax Mwanamke kujitokeza kuchukuwa wageni, jambo ambalo ni lakujivunia.


Hata hivyo aliwataka wanawake wengine kujitokeza, katika kumuunga mkono Shemsa katika mkazi yake ya Udereva Tax, ili kuachana na dhana mbaya kwamba kazi za udereva ni wanaume tu.

Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, alisema anafarajika sana kuona Zanzibar kuwepo kwa dereva wa kwanza Tax katika kisiwa Cha Pemba.

Kujitokeza kwake ni kuonyesha mfano kwa wanawake wenzake, kutokubweteka na kuchagua kazi za kufanya kwani kazi yoyote ni kazi kitu kizuri ni mtu kupata chumo la halali.

“Shemsa amejitolea kuwa Dereva Tax hapa Pemba, ni mwanamke wa kwanza lakini wenzetu bara utawaona wanawake mpaka makondakta wa mabasi ya mwendo kasi, wapo madereva pia hili ni jambo la kujivunia Pemba” alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Hata hivyo amewataka wanawake wenzake kujitokeza katika kazi na kuacha tabia ya kuchagua kazi, kwani dunia sasa imebadilika kutokana na ukosefu wa ajira.

Mwanaharakati wa Masuala ya Wanawake Pemba kutoka TAMWA, Jitihada Abdalla, alisema upo wa Shemsa ni Jambo la kufurahia, wanawake wameanza kujitambua na kufanya kazi kama walivyo wanaume.

Kitendo cha kuchukuwa watalii ni kitendo kizuri, hii inaonesha wanawake wanaweza wakiwezeshwa pale wanapopatiwa fursa, huku akiwataka wasibweteke na kuona ni watu wakuolewa na kutunza familia, bali wanapaswa kushiriki shuhuli mbali mbali za kijamii ili waweze kupata kipato na kuondokana na utegemezi.

TAMWA imekuwa ikiwapa taaluma wanawake ya kushiriki katika mambo mbali mbali ikiwemo kujitambua, nao wananchango mkubwa katika jamii.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa EMAIL:abdisuleiman33@gmail.com


0718968355.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.