Habari za Punde

China wakabidhi msaada wa madawa

 Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar Xie Xiaowu akimkabidhi Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo msaada wa dawa uliotolewa na Serikali ya China makabidhiano haya yamefanyika Bohari Kuu ya dawa Maruhubi Mjini Zanzibar.
 Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo na Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar  Xie Xiaowu wakisaini hati ya makabidhiano ya dawa zilizotolewa Serikali ya watu wa China.
 Wafanyakazi wa Bohari Kuu ya Dawa Zanzibar na wanafunzi wa fani ya ufamasia wakifuatilia sherehe ya kukabidhiwa dawa zilizofanyika Bohari Kuu ya Maruhubi.
Mkurugenzi wa Bohari Kuu ya Dawa Zanzibar Zahran Ali Hamadi akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuboreka kwa hali ya dawa Zanzibar baada ya Waziri wa Afya Zanzibar kukabidhiwa msaada wa dawa kutoka Serikali ya watu wa China.

Picha na Makame Mshenga-Maelezo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.