Kuwepo kwa usafiri wa ndege ya Abiria ya Airbus A350 kutoka Shirika la Ethiopian
Airlines, na kuunganisha safari zake
hadi Zanzibar, kutapanua wigo wa ujio wa watali nchini.
Ndege
hiyo mpya yenye uwezo wa kuchukua abiria 345, iliyoundwa kwa teknolojia ya juu
zaidi, ni ya kwanza Barani Afrika,
ambapo kwa mara ya kwanza imewasili
katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume, jana ikitokea mjini
Addis Ababa, Ethiopia – Kilimanjaro – Zanzibar.
Lengo
la safari hiyo, ni kuitangaza ndege hiyo, ikiaminika itakuwa na mchango mkubwa
katika uimarishaji wa sekta ya utalii nchini.
No comments:
Post a Comment