Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Dk Shein Akabidhi Vifaa Vya Michezo Kwa Timu za Majimbo ya Pemba leo.

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Pemba                                                                                                            17.03.2017
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein  amewataka vijana wa CCM, Kiswani Pemba kuyatumia mashindano ya mpira wa miguu yalioanzishwa na chama hicho kwa kuendeleza amani,mshikamano udugu, umoja, na mapenzi miongoni mwao na sio kugombana.

Dk. Shein ambaye pia, ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, aliyasema hayo leo huko katika ukumbi Skuli Sekondari ya Fidel Castro, Mkoa wa Kusini Pemba mara baada ya kukabidhi vifaa vya michezo ya vijana kwa ajili ya maandalizi ya Ligi ya Mpira wa Miguu kwa Timu 18 za Kisiwani Pemba ikiwa na lengo la kusherehekea mwaka mmoja tokea kuapishwa kwa Dk. Shein kuwa Rais wa Zanzibar awamu ya pili sambamba na kusherehekea miaka 40 ya kuzaliwa kwa CCM.

Dk. Shein aliwataka vijana wa CCM watakaoshindana katika ligi hiyo kutofanya mashindano hayo kuwa sehemu ya mapambano na kuwataka kufuata sheria na taratibu za mpira wa miguu huku akiwasisitiza kuwafuata sheria 17 za soka duniani ili wacheze vizuri.

Katika maelezo yake, Dk. Shein aliwaeleza vijana hao pamoja na wanaCCM waliohudhuria katika hafla hiyo kuwa michezo ni nidhamu na kuongeza kuwa chama cha CCM ndicho kinachofundisha watu nidhamu, na kutoa pongezi za pekee kwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mohamed Raza kwa kuyadhamini mashindano hayo.

Aidha, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kwa kujipongeza kwa niaba ya Wazanzibari na Watanzania wote kwa jumla kwa Zanzibar kupata uwanachama wa CAF huku akitoa wito kwa viongozi wa ZFA kutambua kuwa huu si wakati wa kulumbana na kupelekana mahakamani.

Alisema kuwa hiyo ni ishara ya kuelekea FIFA hivyo, aliutaka uongozi wa ZFA kuachana na masuala ya kupelekeana mahakani na iwapo watafanya hivyo Zanzibar inaweza kutolewa na kuwa aibu kwa Zanzibar na Jamhuari ya Muungano wa Tanzania kwani juhudi kubwa imepita hadi kufikia hapo.

Dk. Shein alisema kuwa miaka mingi Zanzibar ilikuwa ikitafuta nafasi ya uwanachama wa CAF na hivi sasa tayari imeshakuwa mwanachama halali, hivyo aliwataka viongozi wa ZFA watambue kuwa huu si wakati wa malumbano badala yake ni wakati wa kuhakikisha Zanzibar inarudi katika historia yake ya soka.  

“Kufika hapa tulipofika jana ni jitihada za Zanzibar, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania viongozi mbali mbali wa Serikali na Mpira, sasa kazi iliyobakia kuweka pembeni mambo yasiyostahiki katika michezo”alisema.

“Wapi na wapi masuala ya mpira kwenda mahakamani, wakifanya masihara
hicho chama cha CAF hakitokubali kwa mambo hayo, itakuja kuwa ni aibu
kwa Zanzibar, Fifa hawakubali masuala hayo”alisema.

Aliwataka viongozi wa ZFA kuwa makini na kutambua kuwa wao ni viongozi
kwa ajili ya soka la Zanzibar na kuachana na mambo yao binafsi huku akisisitiza kuwa  ZFA iongoze mpira na kuepukana na masuala ya kisiasa ndani ya chama hicho.

Pamoja na hayo, Dk. Shein aliwataka wanaCCM kuendelea na shughuli zao kama kawaida na wenye kazi kufanya kazi zao, wanaosoma waendelee kusoma na waliokuwa hawana kazi Serikali anayoiongoza imo katika juhudi za kuhakikisha wanapata ajira lakini kubwa ni kuepuka maneno ya kizushi kuwa kuna serikali itakuja kuiondoa madarakani serikali iliyopo ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisisitiza kuwa kauli hizo ni za kuzibeza na kuwataka wanaCCM  wasihadaike na waendelee kukiimarisha chama chao na kueleza kuwa hakuna uchaguzi hadi mwaka 2020 na serikali iliyopo madarakani itaendelea kuongoza hadi uchaguzi huo utakapofika. 

Aidha, Dk. Shein aliwataka vijana na wananchi wote kuwa na utamaduni wa  kufanya mazoezi ili kumuepusha na maradhi yasioambukizika na ndio maana ameiweka Januari mosi ya kia mwaka kuwa ni siku ya mazoezi kitaifa.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Abdalla Juma Abdalla Mabodi, alitumia fursa hiyo kutoa shukurani zake kwa uteuzi huo alioupata hivi karibuni na kuelez furaha yake kwa Zanzibar kupata uwanachama wa CAF kwani hatua hizo ni katika utekelezji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM katika suala zima la michezo.

Alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzbar bado iko madarakani na inaendelea kuongoza nchi na kuwataka wanaCCM nKatika hotuba yake Dk. Shein aliwataka vijana washindane katika mchezo huo na wala wasigombane kwani lengo la michezo pamoja na kuanzishwa  kwa mashindano hayo ni kujenga umoja baina yao.

Dk. Shein aliwataka vijana hao wacheze vizuri ligi hiyo ili kuendelea kukipa heshima na mapenzi chama chao cha CCM na kueleza kuwa Ilani ya chama hicho ina vifungu vinavyoeleza kutekelezwa kwa sekta hiyo ya michezo.

Aliongeza kuwa mashindano hayo yana lengo la kuimarisha chama, kutoa vipaji kwa vijana na kuwataka viongozi wa Majimbo kuwaunga mkono na kuwasaidia vijana wao watakaoshiriki katika ligi hiyo kwani na wao wanawajibu wa kufanya hivyo.

Mapema Mdhamini wa mashindano hayo, Mohammed Raza alisisitiza azma yake ya kuazisha na kuyadhamini mashindano ya mpira wa miguu kwa skuli zote za mikoa yote ya Zanzibar kwa kushirikiana na Serikali pamoja na Wizara husika.

Raza pia, aliahidi kutoa zawadi ya gari kwa mshindi wa kwanza katika mashindano hayo kisiwani Pemba pamoja na kutoa vifaa kwa michezo mengine yote ambayo itashindaniwa mbali na mpira wa miguu ikiwemo mpira wa pete, mpira wa kikapu, mpira wa meza na michezo mengineyo.

Katika taarifa ya Ligi hiyo iliyosomwa na Bakar Hemed Bakari  kuwa lengo la mashindano hayo ni kusherehekea miaka 40 ya kuzaliwa kwa CCM, kuinua vipaji vya vijana katika mchezo wa mpira wa miguu sambamba na kuunga mkono kauli ya Dk. Shein ya kutaka Zanzibar iwe na vuguvugu la michezo kwani wanaamini kuwa hoja hiyo imelenga utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Vijana hao pia, walitoa salamu zao za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazania John Pombe Magufuli  na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa jitihada zao za kupambana na biashara haramu ya madawa ya kulevya na kuahidi kuwa wakiwa wao ni vijana watawaunga mkono viongozi hao katika mapambano hayo.

Mshindi wa kwanza wa mashindano hayo atapata kikombe, gari na nishani ambapo mshindi wa pili atapata milioni tatu na mshindi wa tatu atapata milioni mbili pamoja na zawadi nyengine zitakazotolewa katika mashindano hayo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.