Na Himidi Choko.BLW.
Zanzibar Machi 16, 2017
Spika wa Baraza la
Wawakilishi Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid
amesema mashirikiano ya pamoja kwa
makundi yote yanahitajika ili kupinga
vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia na watoto pamoja na matumiziya dawa za
kulenya hapa nchini.
Akizungumza na wasanii
wa Binti Filamu waliongozwa na Ngumbagme Misayo (Thea) huko Afisini kwake Chukwani, Spika Maulid amesema
vitendo hivyo hivi sasa vinaonekana
kushamiri katika jamii hasa kwa watoto wadogo na wafanyaji wamo katika jamii.
Hivyo Spika Maulid
amesema makundi ya kijamii kama vile viongozi wa dini, wanasiasa na wasanii wanawajibu
mkubwa wa kuelimisha juu ya
madhara ya vitendo hivyo.
Amesema kwa kua makundi hayo
yanaushawishi mkubwa katika jamii ni vyema yakaendelea kutoa elimu juu ya ubaya wa vitendo hivyo hatimae vipungue
na kutokomezwa kabisa.
Amesema miongoni mwa
matokeo mabaya ya vitendo hivyo ni kuathika kwa nguvu kazi kisaikolojia
na maambukizi ya magonywa ya zinaa hivyo suala la udhalilishaji wa kijinsia na watoto pamoja na matumizi ya dawa za kulenya
linafaa kupigwa vita kwa nguvu zote.
Nao wasanii wa Binti
Filamu wamesema wataendelea kuelimisha
jamii juu ya madhara ya vitendo hivyo kwa kutumia majukwaa yao ili kulinusuru taifa na balaa la kuwa na viongozi wasiokua na
maadili hapo baadae.
Mazungumzo hayo pia
yamehudhuriwa na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi ambae pia ni Mwenyekiti
wa Umoja wa Wawakilishi Wanawake zanzibar UWAWAZA mhe Mgeni Hassan Juma.
No comments:
Post a Comment