|
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA
UTAWALA BORA
Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli
S.L.P 2643, DAR ES SALAAM
Simu: +255 22 2135747/8;
2137125; 2135222
Faksi: +255 22 2111281
Tovuti: www.chragg.go.tz
|
Mei 8,2017
SALAMU ZA RAMBIRAMBI
TUME ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imepokea kwa majonzi makubwa taarifa ya vifo
vya ghafla vya Wanafunzi 32, Walimu wawili (2) wa Shule ya Lucky Vincent pamoja
na dereva vilivyotokea Mei 6, 2017 asubuhi baada ya basi dogo walilokuwa
wakisafiria kupata ajali katika eneo la Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu, Mkoani
Arusha.
Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora inaungana na Watanzania wote kuomboleza vifo hivyo vya
ghafla vya wapendwa wetu hawa. Huu ni msiba mzito siyo tu kwa shule, wazazi na
wanafamilia bali kwa taifa zima.
Vifo hivyo
vimekatisha haki ya uhai ya marehemu wote na pia imekatisha haki ya elimu ya
wanafunzi hao.
Tunatoa pole
kwa wafiwa wote – wazazi, wanafunzi, waalimu, uongozi wa Shule ya Lucky Vincent
na Watanzania Wote. Mungu awatie nguvu, awape
subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.
Ni wazi kuwa
ajali hiyo imezima ndoto za watoto waliotarajiwa kuwa wajenzi wa taifa wa siku
zijazo; lakini lililo muhimu kwa sasa ni kuwaombea marehemu wote pumziko jema. Aidha Tume inawaombea majeruhi uponaji wa
haraka.
Tume
inaipongeza Serikali kwa jinsi ilivyojitoa katika kusimamia taratibu zote za
kufanikisha mazishi ya marehemu hao.Tume inaiomba Serikali kupitia vyombo vyake
wafanye uchunguzi wa kina wa ajali hiyo, na
matokeo yake yatumike kuepusha ajali nyingine zinazoweza kutokea.
Mwenyezi Mungu aziweke Roho za Marehemu wote mahali pema peponi,
Amina.
Imetolewa na: SIGNED
Bahame Tom Nyanduga
Mwenyekiti
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
Mei 8, 2017
No comments:
Post a Comment