Na Abubakar Kisandu Mwanza.
Timu ya Mpira wa Kikapu (Basketball) ya Pemba imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kuwatoa mabingwa watetezi timu ya Pwani kwa vikapu 33-32 kwenye Mashindano ya Michezo na Sanaa ya Skuli za Sekondari Tanzania (UMISSETA) katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba huko mkoani Mwanza.
Pemba ikiwa mara yake ya kwanza kushiriki Mashindano hayo inaonekana imepania kubeba Kombe hilo baada ya muendelezo mzuri kwa kushinda michezo yake yote kwenye mashindano hayo.
Walianza kushinda vikapu 64-21 dhidi ya Manyara, kisha wakaichapa Rukwa kwa vikapu 41-18 na leo kuwatupilia mbali mabingwa watetezi Pwani kwa vikapu 33-32.
Sasa Pemba wanasubiri kucheza hatua ya Nusu fainali katika mchezo huo wa Kikapu.
No comments:
Post a Comment