NA HAJI NASSOR, PEMBA
JUMLA ya wakulima 2,934 wa zao la karafuu kisiwani Pemba,
sambamba na taasisi sita zikiwemo za serikali na za watu binafsi,
zimeshakabidhiwa miche bure zaidi ya 90, 000 ya mikarafuu kutoka Kitengo cha
Mashamba ya Misitu na Vitalu Pemba, ili kuiotesha kwenye maeneo yao.
Awali
kitengo hicho katika mwaka huu wa 2016/2017, kilipanga kugawa miche hiyo 89,524,
kutoka kwenye vitalu vikuu sita vilivyopo kisiwani Pemba, ingawa lengo hilo
limevuukwa.
Taarifa
zinaeleza kuwa, wilaya ambayo wakulima wamejitokeza kwa wingi ni Chakechake kwa
kufikia 1,390 ambapo waligawiwa miche 29,806, ambapo awali waliomba miche 26,408
na kuvuuka lengo lao.
Wilaya
nyengine ambayo wakulima waliojitokeza kwa wingi ni Mkoani 723, sawa na idadi
ya miche 20,400, ingawa awali waliomba miche 24,570 na kuwa na upungufu wa
miche 4170.
Wilaya ya Wete wakulima 533, wakigawiwa miche 19,146 na Micheweni mkoa wa kaskazini
kisiwani Pemba, ni wakulima 288 ambao walibahatika kugawiwa miche 9,369 ingawa
waliomba miche 10,728.
Akizungumza
kwa njia ya simu, mkuu wa kitengo hicho kisiwani humo, Hamad Omar Said, alisema
kabla ya kuigawa miche hiyo, huwataka mabwana shamba wa wilaya husika, kuyangua
mashamba ya wakulima husika.
Alisema
lengo la kufanya hivyo ni kuepusha mkulima kupewa miche mfano 200, wakati
shamba lake kitaalamu linahitaji miche 150 au zaidi ya alioomba.
“Jengine
tunalilofanya kabla ya kuigawa miche hiyo, wakulima lazima wapitie kwa masheha
ili wajaze fomu maalum, ambayo ndio sisi inayotuongoza kwenye
maombi’’,alifafanua.
Aidha
Mkuu huyo wa Kitengo alisema ingawa wapo baadhi ya wananchi, huomba baada ya
kufunga maombi yao ya awali, na hujitokeza wakati wa ugawaji na ndio maana kuna
ongezeko la miche.
Hata
hivyo alisema Shirika la Taifa la Biashara la ZSCT likiwa ndio mdau mkuu
aliomba miche 2,000 ingawa lilikabidhiwa miche 1,000, samba mba na Jumuia za
kiraia na zile za serikali zilioomba miche 1,100 na kubahatika miche 1,230.
Katika
hatua nyengine Mkuu huyo wa Kitengo, alisema hata zoezi la upandaji miti
kitaifa, ulitengea miche 400 huku mashamba wa serikali likiwemo la Makuwe,
lilitengewa miche 1500 ya mikarafuu, ikiwa ni hatua ya kuyaimarisha.
Mmoja
kati ya wananchi wa Wambaa waliokabidhiwa miche hiyo Amina Haji Makame, alisema
pamoja na utoaji huo bure wa miche, ni vyema wakapewa na elimu.
“Elimu
ya kuitunza na kuiendeleza ni jambo jema, maana inawezekana wapo tunaoichukua tu,
kwa sababu inatolewa bure sasa lazima na elimu ya kuitunza tupewe”,alishauri
Nae
Khadija Hassnuu Mshamba wa Mizingani, aliipongeza serikali kwa kuendelea na
utaratibu huo kwa zaidi ya miaka mitano sasa, jambo ambalo, ni njia moja ya
kuliimarisha zao hilo.
Hata
hivyo baadhi ya wananchi wamesema, utaratibu wa kupitia kwa masheha ili kupata
miche hiyo, inaweza kuwakosesha wengi kutokana na siiuntafahamu iliopo.
Kitengo
cha Mashamba ya Misitu na Vitalu kisiwani Pemba, kimeanza utaratibu wa ugawaji
miche ya mikarafuu bila ya malipo kwa zaidi ya miaka mitano sasa, ikiwa ni njia
moja wapo ya kunyanyua hadhi ya zao hilo.
No comments:
Post a Comment