Habari za Punde

Kaimu Katibu Mkuu UVCCM. Mhe. Shaka Ziarani Kisiwani Pemba ya Kikazi Kukagua Maendeleo ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2015-2020 Pemba.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba Ndg Abdallah Rashid Ali akielezea namna Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inavyotekeleza ilani ya CCM mbele ya Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Mara baada ya kuzuru katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza na maafisa wa serikali pamoja na  Viongozi Mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake Mara baada ya kuzuru katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC)(kulia) akizungumza na viongozi wa kikundi cha Vijana wa Jasiriamali  wa mboga mboga (Mtaji wa masikini)wadi ya pujin mara maada ya kukagua mazao mbali mbali yanayolimwa na kikundi hicho.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba Ndg Abdallah Rashid Ali (kulia)akielezea jambo kwa  Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza mara baada ya kumaliza kukagua mradi wa kikundi cha Vijana wa Jasiriamali  wa mboga mboga (Mtaji wa masikini)wadi ya pujin
Meneja Mradi wa Barabara yenye urefu wa km 35  ya ole ngeneja  Amin khalid abdallah akitoa ufafanuzi juu ya maendeleo ya mradi huo kwa  ndg:Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) alipokwenda kukagua ujenzi wa barabara hiyo.
Daktari dhamana katika hospitali ya chakechake Dkt.Ali Habib Ali akimpokea ndg: Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) alipowasili hospitalin hapo kuangalia wagonjwa na kuwafariji.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akimpatia baadhi ya vifaa tiba mama mzazi wa mtoto Bi,Salha Issa Nassor alipokwenda kuangalia wagonjwa na kuwafariji katika hospitali ya Chake chake wilayan chakechake.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC(KWANZA KULIA)) akiwasili katika ukumbi wa mkutano Tawi la CCM Wawi kuzungumza na Vijana wa CCM wilayani Chake Chake Mkoa wa Kusini pemba
 Vijana wakifuatilia mkutano huo.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza na Vijana wa CCM wilayani Chake Chake Mkoa wa Kusini pemba katika ukumbi wa mkutano Tawi la CCM Wawi
 ''Watumishi wa umma mmepewa dhamana kubwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe.Dkt,John Pombe Magufuli na Rais wa Zanzibar DktAli Shein hivyo ni matarajio ya chama cha mapinduzi na serikali,watumishi wote kusimamia na kuwajibika ili kutekeleza ilani kwa uimara''Alisema ndg: Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC)  wakati akizungumza na maafisa wadhamini,wadhamini wa mabaraza ya mji na madiwani,katika ukumbi wa skuli ya chekechea mdungu wilayani Chake Chake Mkoa wa Kusini pemba.
 Maafisa wadhamini,wadhamini wa mabaraza ya mji na madiwani wakimsikiliza ndg: Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC)
''Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo chini ya CCM hinyo kila kiongozi alieajiriwa na serikali ana jukumu moja kubwa la kutekeleza ilani kwa maslahi mapana na umakini mkubwa''Aliendelea kusisitiza ndg: Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC)  wakati akizungumza na maafisa wadhamini,wadhamini wa mabaraza ya mji na madiwani,katika ukumbi wa skuli ya chekechea mdungu wilayani Chake Chake Mkoa wa Kusini pemba.
(Picha na Fahadi Siraji)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.