Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al Hajj Dk Ali Mohamed Shein Azungumza na Mashekhe wa Wilaya ya Magharibi Unguja Kabla ya Kulihutubia Bara za la Eid Al Hajj katika Viwanja Fumba Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Sheria Katiba na Utawala Bora Mhe. Haroun Ali Suleiman akizungumza na kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al Hajj Dk Ali Mohamed Shein, kuzungumza na mashekhe wa Wilaya ya Magharibi Unguja katika ukumbi wa moja ya nyumba za kisasa fumba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al Hajj Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza na Mashekhe wa Wilaya ya Magharibi Unguja kabla ya kuaza kwa Baraza la Eid Hajj lililofanyika katika viwanja vya fumba Zanzibar. 
Baadhi ya Viongozi wa Dini kisiwani Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza na Mashekhe wa Wilaya ya Magharibi Unguja.
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji akisoma dua baada ya hafla ya mazungumzo na Rais wa Zanzibar Dk Shein.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.