JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI
YA RAIS
TAWALA
ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.
George Simbachawene anawajulisha wazazi, walezi na wananchi wote kuwa
Mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi itafanyika tarehe 6-7/09/2017 kwa
kuzingatia sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa na Baraza la Mitihani
Tanzania.
Kwa mwaka huu wa 2017
jumla ya wanafunzi watakaofanya mitihani hiyo ni 917,030 kutoka katika shule za
Msingi 16,581 ambazo ni za Serikali na
binafsi zilizoko Tanzania Bara.
Maandalizi ya
uendeshaji na usimamizi wa Mitihani hii umekwishakamilika katika ngazi zote
ikiwa ni pamoja na kusafirishwa kwa mitihani na wasimamizi kutoka ngazi ya
halmashauri kwenda kwenye vituo vya kufanyia mitihani na fedha kwa ajili ya
gharama za usimamizi na uendeshaji wa mitihani.
Gharama zitakazotumika
hadi kukamilika kwa zoezi la Mitihani ya darasa la saba ni Tsh Bil
29,474,964,600 na fedha hizo zitatumika kwa ajili ya uendeshaji na usimamizi wa
mitihani tu.
Waziri Simbachawene
amewaagiza Wakurugenzi wote Nchini kutumia Fedha hizo zilizopokelewa kwa ajili
ya mitihani kwa kufuata muongozo na kuhakikisha wanakamilisha mahitaji yote na
kuwalipa wasimamizi staili zao ili waweze kufanya kazi hii kwa moyo na kwa uadilifu.
Aidha Waziri
Simbachawene amewatakia heri na baraka watahiniwa wote watakaoanza mitihani yao
hapo kesho na kuwataka kuwa watulivu katika kipindi chote cha Mitihani na
kufuata taratibu na maelekezo ya wasimamizi.
Imetolewa
na:
Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi
ya Rais
Tamisemi.
No comments:
Post a Comment