Na.Haji.Nassor- Pemba.
IJAPOKUWA
kuanzia serikali za wilaya, mkoa hadi taifa zimeshapiga marufuku kwa wanawake,
watoto na watu wengine kuacha kabisa kuokotoa karafuu zinazoanguka “mpeta”
lakini bado wengine wanaendelea kupuuzia agizo hilo.
Wapo
wanaoendelea kuokota mpeta wakiwa na watoto wao, ingawa sababu za kuokota mpeta
wenyewe huwa wanazo na pengine ukizisikiliza zina akili.
Maana
wengine husema kama ni vitendo vya udhalilishaji, bsi vipo hata kabla ya ujio
wa zao hili la karafuu, na ndio maana wanadai kuwa anaetaka kudhalilishwa hata
kama hakuna karafuu.
Lakini
kubwa na lililonileta mbele yenu leo hii na kuutumia ukurasa huu, ni kuwauliza
hawa wanaokwenda kuokota mpeta wakiwa wamejipamba wana ajenda gani huko?
Maana
utashangaa wakati ukipishana nao au kama utabahatika kupanda gari moja nao,
jinsi walivyojipura kama sio kujiremba.
Kiutamaduni
kila mmoja anaekwenda kazini hukoga na kujipura jinsi awezavyo, ingawa kila ina
mazingira yake, lakini sio kuokota mpea na kujipambana mbona kama haifanani
hivi.
Kumbe
lile wazo na agizo la serikali kupiga marufuku uokotaji mpea kwamba kunaongeza
kasi ya udhalilishaji, inaweza sasa kuiingia akili, maana iweje mtu anakwenda
msituni lakini awe sawa na anaekwenda harusini?
Kwa
haraka inawezekana usiamini, kwamba wapo akinamama wajane, wari na hata wake za
watu lakini wapotoka kwenda huko kunakoitwa kuuokota mpeta, basi hutamani
kuwapisha.
Sujui
niende mbali zaidi, kwamba inawezekana mpeta unaotafutwa ni huu wa udhalilishaji
au kujipamba huko ni asili ya mtu kusudi, kama hivyo ndivyo basi punguzeni.
Jengine
ambalo naendelea kujiuliza kwa kujipamba huko tena, mtu mmoja hukata kundi kila
wanapofika kwenye mashamba ya mikarafuu, akidai kuwa kufuata na na watu
huzipati.
Jamani
neema hii ya karafuu aliotujaalia Allah, sisi waokotaji mpeta na wachumaji
tunataka kuichanganya na uovu wa zinaa, jamani huko sio kwa kwenda maana kuna
la leo na kesho.
Akinamama
hawa na watoto wenye umri tofauti, unaweza kuwashangaa wanaporudi kuokota mpeta, wakiwa na zaidi ya pishi moja, ambayo
kimtazamo hilo kwa mpeta wasasa haliwezekani.
Yote
kwa yote, jamani wanawake nyinyi ambao mnafuata misingi na madhehebu ya
kiislamu ni sahihi hilo mnalolifamnya la kujipamba kwa rangi, asumini na hali
uudi mnapokwenda kuokota mpeta?
Kwa
hili sasa lazima wanaume ambao ndio wasimamizi wakuu wa nyumba na familia zetu,
lazima tujiridhishe na hili maana tumeshaelezwa kuwa, kila mmoja ataulizwa kwa
alilolichunga.
Wanawake
wenyewe hebu rudini kwa Muumba wetu na wengine kuheshimu ndoa au dini yetu,
maana maandishi yasio na shaka yanaeleza
wapi na wakati gani mwanamke ajipambe.
Na
nyinyi mnaochuma (vibarua) acheni mtindo na tabia ya kuwamiminia karafuu
wanawake ambao wengine wako kwenye ndoa, kisha malipo yawe ya udhalilishaji
“mali kwa mali” sio jema hilo.
Lakini
viongozi wa dini, serikali wa shehia na taifa endeleeni kulikemea hili la
uokotaji mpeta tena usio salama, maana inawezekana baada ya kumalizika watoto
wanaoitwa wa mzazi mmoja kuongezeka.
Naamini
kila kitu kinawezakana ikiwa kila mmoja atatekeleza wajibu wake bila ya
kusimamiwa na rushwa ikawa mwiko.
Mwandishi hajinassor1978@gmail.com
No comments:
Post a Comment