Mkurugenzi wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na
Teknolojia, Zanzibar Abdulhamid Idrissa Haji (kushoto) akizungumza na waandishi
wa habari (hawapo pichani) mjini Zanzibar mwishoni mwa juma wakati wa hafla ya
kupokea majenerata matatu kutoka Zantel yatakayowasaidia wanafunzi wa chuo
hicho katika masomo yao kama mbadala wa nishati hasa kipindi ambacho Umeme
umekatika.
Mkuu wa Zantel, Zanzibar Mohamed Mussa Baucha, akizungumza
na waandishi wa habari mjini Zanzibar mwishoni mwa juma wakati wa hafla ya
kukabidhi majenerata matatu kwa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia,
Zanzibar ambayo yatawasaidia wanafunzi wa chuo hicho kwenye masomo yao kama
mbadala wa nishati katika kipindi ambacho
Umeme umekatika.
Mkuu wa Zantel, Zanzibar Mohamed Mussa Baucha, akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kukabidhi majenerata matatu kwa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, mwishoni mwa juma mjini, Zanzibar. Majenereta hayo yana lengo la kuwasaidia wanafunzi wa chuo hicho kwenye masomo yao kama mbadala wa nishati katika kipindi ambacho Umeme umekatika. Pamoja nae tokea kushoto ni Afisa Mkuu wa Biashara Zantel, George Lliakopoulos, Afisa Mkuu wa Masuala ya Fedha Zantel, Jean-Paul Happart na Kulia ni Afisa Mkuu wa Masuala ya Ufundi na Teknolojia Zantel, Larry Arthur.
Mwanafunzi wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, Zanzibar Abdukadir Mkubwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar mwishoni mwa juma wakati wa hafla ya kupokea majenerata matatu kutoka Zantel yatakayowasaidia wanafunzi wa chuo hicho katika masomo yao kama mbadala wa nishati hasa kipindi ambacho Umeme umekatika.
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, Zanzibar Abdulhamid Idrissa Haji
(katikati) akimpongeza Afisa Mkuu wa Masuala ya Ufundi na Teknolojia Zantel,
Larry Arthur hivi karibuni mjini Zanzibar na kumshukuru kwa msaada mkubwa ambao
Chuo hicho wameupata kutoka Zantel. Zantel walikabidhi msaada wa majenerata
matatu yatakayowasaidia wanafunzi wa chuo hicho katika masomo yao kama mbadala
wa nishati hasa kipindi ambacho Umeme umekatika
ZANTEL imetoa msaada wa majenereta
tatu zilizotumika kwa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, Zanzibar
mwishoni mwa juma mjini Unguja.
Majenereta hayo yenye
ambayo yamekwishatumika yenye thamani ya dola 250,000 yamekabidhiwa kwa Taasisi
hiyo ili kusaidia jitihada za Chuo hicho katika kuhakikisha wanafunzi wanaendelea
na masomo yao kipindi ambacho Umeme umekatika.
Akizungumza wakati wa
hafla ya makabidhiano mwishoni mwa juma mjini Unguja, Mkuu wa Kampuni ya
Zantel, Zanzibar, Ndugu Mohamed Mussa Baucha alisema mchango huo una lengo la
kuwasaidia wanafunzi wa chuo na masomo yao kama mbadala wa nishati hasa kipindi
Umeme unapokua umekatika huku akitumai kwamba wanafunzi wa chuo hicho, watahimizwa
kufanya vizuri kutokana na msaada huo.
"Ni jambo la furaha
na faraja kwetu kutoa msaada wa majenereta kwa Taasisi hii, na tumaini letu
kubwa ni kuwa yatakuwa msaada muhimu kwa wanafunzi katika masomo yao,"
alisema Baucha.
Aliongeza kuwa ZANTEL
imekuwa msatari wa mbela katika kujitolea na itaendelea kuwekeza katika miradi
mbalimbali endelevu na kuunga mkono mipango inayozingatia kuboresha elimu
nchini.
Abdulhamid Idrissa Haji,
ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo alisema kuwa msaada huo umekuja kwa
wakati muafaka kwa sababu chuo chake hakikuwa na vyanzo mbadala vya nishati,
mara umeme unapokuwa umekatika, kitu ambacho kiliwasababishia wanafuzi wengi
usumbufu.
"Ukosefu wa umeme
vyuoni, hukatisha morali ya wanafunzi hasa hasa kwa masomo ya sayansi na uwezo
wa kuyaelewa masomo hayo kwa usahihi."
Aliishukuru Zantel kwa
msaada wao muhimu katika kuboresha ubora wa elimu nchini na kuhimiza makampuni
mengine kufuata mfano huo.
“Msaada huu sio chachu tu
katika ufaulu wetu kitaaluma bali pia utaongeza morali kwa wanafunzi,”
alihitimisha Haji.
Mwanafunzi wa chuo hicho
aliyefahamika kwa jina Abdulkadir Mkubwa Khamis ambaye anachukua masomo ya
sayansi, alisema mchango wa Zantel utawawezesha kuboresha utendaji wao na pia
kutatua baadhi ya changamoto ambazo zilikuwa zinawakabili hapo awali.
"Matatizo ya umeme
huathiri sana masomo yetu, lakini kwa msaada huu, natumai matatizo hayo
yatapungua," alihitimisha.
Mwaka jana, Kampuni ya
Zantel ilitoa vitabu vyenye thamani ya 10M/- kwa Taasisi hiyo katika jitihada
za kupunguza uhaba wa vifaa vya kufundisha na kujifunzia chuoni hapo.
KWA MAELEZO ZAIDI:
Rukia Mtingwa
Baruapepe:
r.mtingwa@zantel.co.tz
Tovuti: www.zantel.com
No comments:
Post a Comment