Habari za Punde

MASAUNI AFANYA MKUTANO WA HADHARA KILWA KUSINI ASISITIZA ADHMA YA SERIKALI KUKOMESHA UHALIFU NCHINI

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kilwa Kusini(hawapo pichani), wakati wa mkutano wa hadhara ambapo aliwaasa wananchi hao kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama kufichua wahalifu ikiwa ni kuisaidia serikali katika adhma ya kukomesha matendo ya uhalifu nchini.Mkutano huo umefanyika katika Viwanja vya Maalim Seif,Kilwa Kusini
 Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi, Christopher Ngubiagai akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kilwa Kusini(hawapo pichani), wakati wa ziara ya Naibu Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni.Mkutano huo umefanyika katika Viwanja vya Maalim Seif,Kilwa Kusini.
Mwananchi wa Kilwa Kusini, Said Saleh, akimuuliza swali Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), kuhusu kukamatwa na polisi  kwa ndugu zao wanaotuhumiwa kwa uhalifu.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 
 Mwananchi wa Kilwa Kusini, Rehema Said , akimuuliza swali Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), kuhusu uhalifu wanaofanyiwa wanawake ikiwemo kubakwa na kuporwa pesa na mali na wahalifu
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Kilwa Kusini baada ya kumaliza mkutano wa hadhara ambapo aliwaasa wananchi hao kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama kufichua wahalifu ikiwa ni kuisaidia serikali katika adhma ya kukomesha matendo ya uhalifu nchini.

Wananchi wa Wilaya ya Kilwa wakimsikilza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara ambapo aliwaasa wananchi hao kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama kufichua wahalifu ikiwa ni kuisaidia serikali katika adhma ya kukomesha matendo ya uhalifu nchini.Mkutano huo umefanyika katika Viwanja vya Maalim Seif,Kilwa Kusini.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA   SERIKALI -WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.