Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Naibu Waziri wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Lulu Msham Abdallah, hafla hiyo imefanyika Ikulu Zanzibar leo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi
aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar.
Hafla hiyo, ilifanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi
mbali mbali wa Serikali ambapo viongozi walioapishwa ni Lulu Mshamu Abdalla kuwa
Naibu Waziri wa Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Joseph Abdalla
Meza kuwa Kamishna wa Bodi ya Mapato ya Zanzibar (ZRB).
Dk. Shein amewaapisha
Makatibu Wakuu ambao ni Ali Khalil Mirza kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi,
Nyumba, Maji na Nishati, Omar Hassan
Omar aliapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo,
Dk. Idrissa Muslim Hija ameapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Amali.
Pia, Dk. Shein amemuapisha Khadija Bakari Juma
kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Juma Ali Juma
ameapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda,
Aidha, Dk. Shein amemuapisha Maryam Juma Abdalla
Saadalla kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Shaaban
Seif Mohamed kuwa Katibu Mkuu katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
Kwa upande wa Naibu Makatibu Wakuu, walioapishwa
ni Tahir Mohammed Khamis Abdulla kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati,
Ali Khamis Juma kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda, Ahmad Kassim Haji kuwa Naibu Katibu Mkuu katika
Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi.
Pia, Dk. Shein amemuapisha Dk. Amina Ameir Issa
kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale
anaeshughulikia masuala ya Utalii na Mambo ya Kale, Mwanajuma Majid Abdulla
ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee,
Wanawake na Watoto anaeshughulikia masuala ya Wazee, Wanawake na Watoto.
Wengine ni Maua Makame Rajab ameapishwa kuwa Naibu
katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wanawake na Watoto anaeshughulikia
masuala ya Kazi na Uwezeshaji, Amour Hamil Bakari kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara
ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Dk.
Saleh Yussuf Mnemo kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya
Kale anayeshughulikia masuala ya habari.
Viongozi mbali mbali
walihudhuria katika hafla hiyo akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir
Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar
Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri na
Manaibu Mawaziri.
Viongozi wengine
waliohudhuria ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini
Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib
Abrahman Khatib, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih,Kadhi Mkuu wa
Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Washauri wa Rais wa Zanzibar pamoja na viongozi
wengine wa Serikali.
Nao viongozi hao walioapishwa
waliahidi kuendelea kumsaidia Rais Dk. Shein katika kuhakikisha Zanzibar
inazidi kupata maendeleo endelevu na kusisitiza ushirikiano katika utendaji wa
kazi ili malengo yote yaliokusudiwa yaweze kufikiwa ikiwa ni pamoja na
kuwatumikia wananchi na kuwasogezea huduma zote muhimu za kijamii.
Kufuatia mabadiliko ya Wizara za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar yaliofanyika hivi karibuni, Rais Dk. Shein alifanya
uteuzi na kuwabadilisha wadhifa baadhi ya watendaji wakuu katika taasisi mbali
mbali za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422
Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment