Kipa wa timu ya Uchukuzi, Willy Barton jana akidaka
mpira katika mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika kwenye uwanja wa Chuo Kikuu
Kishiriki cha Mkwawa wakiajiandaa na mechi za mashindano ya Kombe la Mei Mosi
yanayofanyika kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa
Mchezaji Sharifa
Hamis (kulia) akifanya mazoezi ya kucheza bao na Ambakisye Mwasunga (kushoto)
wakifanya mazoezi ya kujiandaa na michuano ya Mei Mosi kwa upande wa michezo ya
jadi inayofanyika kwenye uwanja wa Somora mkoani Iringa. Katikati ni mchezaji
wa mchezo wa draft Bw. Omar Said akiangalia
Beki Nestory Tweve (3) wa timu ya Tumbaku ya
Morogoro akitafuta njia ya kuwapita Francis Singa na Abdul Kawamba (wenye jezi
nyeusi) wa RAS Iringa, katika mchezo wa mashindano ya Kombe la Mei Mosi
uliofanyika jana kwenye uwanja wa Samora. Tumbaku walishinda magoli 3-0
Mfungaji
Fatuma Machenga (GS) wa Ikulu akifunga mbele ya mlinzi wa RAS Iringa (GK),
Maria Mwita katika mchezo wa netiboli wa mashindano ya Kombe la Mei Mosi
uliofanyika jana kwenye uwanja wa Chuo Kikuu cha Katoliki (RUCO) Iringa.
Ikulu wameshinda magoli 49-8.
Mlinzi wa pembeni Ester Turuka (WA) wa RAS
Iringa akirusha mpira kwa mfungaji wao Warda Sapal (GS) huku mlinzi Lilian
Sylidion (GD) wa Ikulu akijitahidi kuzuia katika mchezo wa netiboli wa
mashindano ya Kombe la Mei Mosi uliofanyika jana kwenye uwanja wa Chuo Kikuu
cha Katoliki (RUCO) Iringa. Ikulu wameshinda magoli 49-8.
Na
Bahati Mollel-TAA, Iringa
TIMU
ya Ofisi ya Rais Ikulu imewachapa bila huruma wenyeji RAS Iringa kwa kuwafunga
magoli 49-8 katika mchezo wa netiboli wa michuano ya Kombe la Mei Mosi
uliofanyika kwenye uwanja wa Chuo Kikuu cha Katoliki (RUCO) mkoani Iringa.
Ikulu
inayofundishwa na kocha mzoefu Mary Protas ambapo wafungaji wake Fatuma
Machenga aliibeba timu yake kwa kufunga magoli 48 huku Irene Elias alifunga bao
moja pekee. Magoli ya RAS Iringa yamefungwa na Warda Sapal na Zitaamanzia
Kididi kila mmoja manne.
Katika
mchezo wa soka timu ya RAS Iringa ilifungwa na Tumbaku ya Morogoro kwa magoli
3-0 katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja w Samora.
Washindi
walipata bao lao la kwanza kupitia kwa Ramadhani Shegodo aliyefunga dakika ya
tisa baada ya kupata pasi kutoka kwa Mohamed Mtawal; huku bao la pili
lilipatikana dakika ya 29 kwa shuti kali
la Ushindi Nzogela.
Bao
la tatu lilifungwa na Salum Idd katika dakika 52 baada ya kupiga krosi murua
iliyomshinda kipa Mashaka Peter aliyejikuta akiusindikiza mpira langoni mwake.
Hatahivyo,
Tumbaku itabidi wajilaumu kwa kukosa magoli mengi ya wazi, ikiwemo dakika ya 20
mshambuliaji wake Issa Simbaliana kukosa penalti iliyotolewa na mwamuzi Steven Makuka baada ya
Nzogele kuchezewa rafu na Dickson Kiboye wa RAS Iringa, lakini kwa kupaisha
mpira juu ya goli,
Timu
za mchezo wa netiboli zitacheza kwa mtindo wa ligi kutokana na kuwa tano,
ambazo ni Uchukuzi, Ikulu, Hifadhi ya Ngorongoro, Shirika la Umeme Tanzania
(Tanesco) na RAS Iringa, ambapo bingwa atapatikana kwa wingi wa pointi na
magoli ya kufunga.
Kwa
upande wa soka timu zimegawanywa katika makundi mawili, ambapo kundi ‘A’ linaundwa
RAS Iringa, Tumbaku, Tanesco na Hifadhi ya Ngorongoro, huku kundi ‘B’ zipo
Geita Gold Mine (GGM), Uchukuzi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Ofisi ya
Taifa ya Ukaguzi (NAO).
No comments:
Post a Comment