Habari za Punde

Mabingwa wa Tamasha la Utalii Utamaduni, Biashara na Michezo Pemba Timu ya New Star ya Wete.


Na Abdi Suleiman -Pemba.

Timu ya New Star ya Wete hatimae imefanikiwa kutwaa 

ubingwa wa Tamasha la Utalii, Utamaduni, Biashara na 

Michezo Pemba, baada ya kuifunga Timu ya Mwenge kwa 

mikwaju ya Penant 3-2.


Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa michezo Gombani, 

huku ukihudhuriwa na mashabiki wengi wa soka uwanjani 

hapo, awali timu hizo zilimaliza dakika 90 zikiwa 

zimefungana bao 1-1.


Fainali hiyo iliyowakutanisha watoto wa Mjini wete, iliweza 

kuvuja hisia za mashabiki wa soka, kutaka kuiyoa Mwenge 

itaendelea kuwa mteja wa New Star, kwani timu hiyo imekua 

ikizisumbua Jamhuri na Mwenge kila zinapokutana.


Kumalizika kwa mchezo huo Kocha wa Timu ya New Star, 

Ustadhi Yahya Ali  alisema ushindi huo umetokana na 

wachezaji wake kukubalia kucheza mpira na kuepuka kiingia aibu ya kufungwa na Mwenge.


Alisema mwenge ni timu Kubwa na katika Wete, hivyo 
ataendelea kuiheshimu kila watakapokutana lakini 
wasitegemee kuifunga New Star kila watakapokutana.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.