Habari za Punde

Wanamichezo Kisiwani Pemba Watakiwa Kutumia Vifaa Vya Michezo na Vyakula Bora.


Na.Abdi Suleiman -Pemba.

MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Viwango Zanzibar 

Khatib Mwadini Khatib, amewataka wanamichezo Kisiwani 

Pemba kuhakikisha wanakula na kutumia vifaa vya michezo, 

ambavyo vimechunguzwa na Taasisi ya Viwango Zanzibar ili 

kulinda afya zao.


Alisema pindi wanamichezo wakitumia vitu ambavyo 

vimechunguzwa na Taasisi hiyo, wataweza kuepukana na 

maradhi mbali mbali yataweza kuua viwango vyao.


Mkurugenzi huyo alitoa kauli hiyo wakati wa kukabidhi 

zawadi kwa washindi wa marathoni katika Viwanja vya 

michezo Gombani, ikiwa ni tamasha la Utalii, Utamaduni, 

Biashara na Michezo Pemba.


Alisema serikali imekuwa ikiwategemea wanamichezo katika 

kuutangaza utalii wake ndani na nje ya nchi, wanamichezo 

wananafasi kubwa ya kutumia vyakula ambavyo 

vimepitishwa na taasisi ya ZBS.


“Siku hizi kumekua na bidhaa mbali mbali zinaingia nchini 

ikiwemo vitu vya mitumba, vizuri wanamichezo kutumia vitu 

ambavyo vimepitishwa na taasisi yetu ya viwango Zanzibar, 

ili kulinda afya zetu kutokana na umuhimu wetu katika 

nchi”alisema.


Alisema serikali imekua mstari wa mbele katika kuinua 

michezo, haipendezi leo kuona wachezaji wanashindwa 

kufikia malengo yao kutokana na kutumia vifaa na kula 

chakula ambacho hakina kiwango.


Hata hivyo aliwapongeza wanamichezo wote walioshiriki 

katika mashindano ya Marathoni, ikizingatiwa michezo ni 

ajira, udungu, urafiki na afya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.