Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Bw.James Coasta,C.H.A. Mkurugenzi Mkuu wa Hoteli ya Discovery Kartika Plaza iliyopo katika Mji wa Bali Nchini Indonesia mara baada ya kuwasili katika Mji huo akiwa na ujumbe wake katika ziara ya kikazi kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohamed Jusuf Kalla,{Picha na Ikulu.] 03/08/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein (katikati) pamoja na Viongozi wengine katika ujumbe wake wakiangalia ngoma za kiutamaduni Mjini Bali nchini Indinesia baada ya mapokezi katika Hoteli ya Discovery Kartika Plaza,katika ziara ya kikazi kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohamed Jusuf Kalla,{Picha na Ikulu.] 03/08/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Gavana wa Mji wa Bali nchini Indonesia Bw.IMade Mangku Pastka kwa mazungumzo katika Hoteli ya Discovery Kartika Plaza alipokuwa katika ziara ya kikazi Nchini Indonesia kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohamed Jusuf Kalla,{Picha na Ikulu.] 03/08/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akiwatambulisha Viongozi aliofuatana nao katika ziara ya kikazi alipotembelea Mji wa Bali kwa Gavana wa Mji huo Bw. IMade Mangku Pastka kabla ya mazungumzo yao yaliyofanyika katika Hoteli ya Discovery Kartika Plaza ziara hiyo ni mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchini Indonesia Mhe. Mohamed Jusuf Kalla,{Picha na Ikulu.] 03/08/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Gavana wa Mji wa Bali nchini Indonesia Bw.IMade Mangku Pastka (katikati) wakiwa katika mazungumzo ya pamoja na Viongozi wengine wa pande zote mbili katika Hoteli ya Discovery Kartika Plaza,Rais alipokuwa katika ziara ya kikazi Nchini Indonesia kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohamed Jusuf Kalla,{Picha na Ikulu.] 03/08/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yao na Gavana wa Mji wa Bali nchini Indonesia Bw.IMade Mangku Pastka yaliyofanyika jana katika Hoteli ya Discovery Kartika Plaza akiwa katika ziara ya kikazi na Ujumbe aliofuatana nao Nchini Indonesia kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohamed Jusuf Kalla,{Picha na Ikulu.] 03/08/2018.
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Bali,
Indonesia 04.08.2018
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameipongeza fursa iliyotolewa na uongozi wa Serikali
wa kisiwa cha Bali ya kwenda kujifunza uendeshaji wa sekta ya Utalii hasa
ikizingatiwa kuwa Bali imepata mafanikio makubwa katika sekta hiyo.
Dk. Shein
aliyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na kiongozi wa Jimbo la Bali (Gavana) I Made Mangku Pastka, mazungumzo
yaliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Kartika Plaza iliyopo mjini Bali.
Katika mazungumzo
hayo, Rais Dk. Shein alimueleza kiongozi huyo kuwa fursa hiyo ni ya pekee na
inajenga imani kubwa kwa Zanzibar kutokana na uhusiano wa kihistoria uliopo
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar na Indonesia.
Alieleza kuwa hatua
hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kutoa fursa kwa wanafunzi wa kada ya utalii
wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kupata nafasi ya
kwenda kujifunza namna ya uendeshaji wa utalii katika kisiwa hicho ambacho
kimepata mafanikio makubwa kutokana na sekta ya utalii kuimarika.
Dk. Shein alitumia
fursa hiyo kutoa shukurani kwa kiongozi huyo kwa mapokezi na makaribisho yake
makubwa aliyomfanyia yeye na ujumbe wake katika kisiwa hicho kiliopo Kusini
Mashariki mwa Jakarta.
Rais Dk. Shein
alieleza kuwa kipindi kirefu Zanzibar imeingia katika shughuli za kitalii ikiwa
na lengo la kukuza uchumi na kuinua pato la Taifa ambapo kwa hivi sasa sekta
hiyo imekuwa ikichangia fedha za kigeni kwa asilimia 80.
Alieleza kuwa
miongoni mwa malengo katika kukuza sekta hiyo kwa upande wa Zanzibar ni
kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 idadi ya watalii wanaotembelea Zanzibar iweze
kupindukia lengo lililokusudiwa la kufikia watalii laki tano kwa mwaka.
Aidha, Rais Dk.
Shein alieleza haja ya Zanzibar kushirikiana na Bali katika kuendeleza sekta ya
uvuvi ambayo nayo imeweza kupata mafanikio makubwa katika kisiwa hicho.
Mapema katika
maelezo yake Kiongozi Mkuu huyo wa Bali alimkaribisha Rais Dk. Shein kiswani
hapo na kumueleza jinsi yeye mwenyewe binafsi pamoja na wananchi wa kisiwa
hicho walivyofarajika kutokana na ujio wa Rais Dk. Shein hatua ambayo inazidi
kujenga uhusiano uliopo kati ya Indonesia na Zanzibar.
Alieleza kuwa
kutokana na shughuli kubwa za kisiwa hicho kuwa ni za kitalii na kupelekea kuwa
na hoteli nyingi za kitalii, vyuo vya kitalii pamoja na kuwepo huduma mbali
mbali zinazotolewa kwa watalii hivyo alimueleza Dk. Shein Zanzibar kuwa wako
tayari kutoa nafasi za kwenda kujifunza huko Bali ili Zanzibar nayo izidi
kuimarika katika sekta hiyo.
Aliongeza kuwa
Bali iko tayari kutoa nafasi za masomo kwa vijana wa Zanzibar wa kada ya utalii
kwenda kujifunza zaidi kisiwani humo na hata kwenda kwa ajili ya kubadilishana
uzoefu na utaalamu.
Pia, kiongozi
huyo alimueleza Rais Dk. Shein mafanikio iliyoyapata Bali katika kuimarisha
sekta ya uvuvi na kuunga mkono kuwepo kwa mashirikiano baina ya pande mbili
hizo.
Akiwa katika
ukumbi wa hoteli ya Kartika Plaza iliyopo mjini Bali, Rais Dk. Shein alikutana
na uongozi wa Kampuni ya Utalii ya Bali ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake
Abdulbakar Mansoer ambaye alieleza mafanikio yaliopatikana katika sekta ya
utalii kisiwani humo huku akiahidi mashirikiano kati ya Bali na Zanzibar.
Wakati huo huo Dk Shein
alitembelea Chuo Kikuu cha Udayana kiliopo Jambaran mjini Bali na kupata fursa
ya kuzungumza na uongozi wa Chuo hicho pamoja na wananfunzi wa chuo hicho
katika ukumbi wa jengo la uongozi wa chuo hicho wa Ruang Bangsa.
Akizungumza na
uongozi wa Chuo hicho Rais Dk. Shein alitoa pongezi na shukurani kwa uongozi wa
Chuo Kikuu cha Udayana kwa mapokezi mazuri waliyomfanyia yye na ujumbe wake
pamoja na kusisitiza haja ya kuwepo kwa mashirikiano kati ya Chuo Kikuu cha
Taifa cha Zanzibar (SUZA) na chuo hicho.
Nao uongozi wa
Chuo Kikuu cha Udayana walieleza kufarajika kwao na ziara hiyo ya Dk. Shein
katika Chuo Chao hicho na kueleza kuwa imefungua ukurasa mpya wa mashirikiano
kati ya Zanzibar na Bali hasa ikizingatiwa kuwa miongoni
mwa masomo makuu ya Chuo hicho ni masomo ya Utalii ambapo tayari Chuo Kikuu cha
SUZA nacho kimeshaanzisha kada.
Akizungumza na
wananfunzi katika ukumbu wa Ruang Bangsa Chuo hapo Rais Dk. Shein aliwasisitiza
kusoma kwa bidii na maarifa hasa ikizingatiwa kuwa nchi yao ya Indonesia
inawategemea kuwa viongozi na watendaji wazuri wa hapo baadae.
Dk. Shein ambaye
pia, ni Makamo Mwenyekiti wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA),
aliwakaribisha wanafunzi hao kuja Zanzibar kujifunza, kutembelea pamoja na
kubadilishana uzoefu na utaalamu na Chuo Kikuu cha SUZA.
Rais Dk. Shein
pia, alikubali wazo la Chuo Kikuu cha SUZA cha Zanzibar kuwa na mahusiano na
Chuo hicho kama ilivyoombwa na uongozi wa chuo hicho na kusisitiza kuwa hatua
hiyo itasaidia katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo baina ya pande
mbili hizo.
Dk. Shein pia,
aliwaeleza historia ya Zanzibar jinsi ilivyoingia katika sekta nzima ya
biashara pamoja na utalii ambao ni sehemu ya maisha kama ilivyo kwa Indonesia ambapo
alieleza kuwa utalii wa Zanzibar uliimarishwa zaidi mara baada ya Mapinduzi
matukufu ya Januari 12, 1964 ambapo sekta hiyo iliwekewa mikakati maalum.
Aidha, Rais Dk.
Shein alaieleza kuwa ukongwe wa Chuo hicho ambacho kimeanzishwa miaka 56
iliyopita uzoefu wake utakuwa msaada mkubwa kwa Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA) iwapo kutakuwa na mashirikiano ya pamoja.
Mara baada ya
kumaliza ziara katika Chuo Kikuu hicho cha Udayana, Rais Dk. Shein alitembelea
ofisi ya Kampuni ya mafuta ya nazi ya
‘Samani Island Virgin Coconut Oil’ ambapo uongozi wa Kampuni hiyo ulimueleza
shughuli inazozifanya pamoja na mafanikio uliyoyapata kutokana na kuwa na soko
la uhakika la mafuta ya nazi la ndni na nje ya nchi ikiwemo Ujerumani,Australia,
Bulgaria, Japan na nchi nyenginezo.
Kwa maelezo ya
Rais Dk. Shein lengo kuu la ziara hiyo katika Ofisi hizo ni kuangalia uwezekano
wa kushirikiana pamoja kampuni hiyo katika kufufua biashara pamoja na kilimo
cha nazi ambacho kiliijengea sifa kubwa Zanzibar hapo siku za nyuma
Rais Dk. Shein
akiwa katika kisiwa hicho cha Bali aliungana na Waislamu ambao ni asilimia
kubwa ya wakaazi nchini Indonesia pamoja na kiswa hicho katika sala ya Ijumaa
iliyofanyika katika Masjid Huda Islamiya Mjini Bali.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment