Na Salum Vuai
JAMII
katika Wilaya ya Kati, imehimizwa kuwasimamia vyema watoto na kuhakikisha
wanasoma vizuri elimu zote, dini na dunia.
Akizungumza
wakati wa mashindano ya kuhifadhi Kuran kwa madrasa za kanda ya Bungi katika
jimbo la Tunguu, Mwakilishi wa jimbo hilo Simai Mohammed Said, amesema elimu ya
dini ndio dira ya kuwaongoa watoto wa Kizanzibari.
Amesema
vitendo vya udhalilishaji vilivyokithiri nchini, vinaweza kudhibitiwa iwapo
kila mzazi atabeba kikamilifu dhima ya uchunga wa familia kwa ushirikiano na
wanajamii wote.
Simai
alieleza kufurahishwa na utaratibu wa kuandaa mashindano hayo ya kuhifadhi
kitabu kitatakatifu cha Mwenyezi Mungu, akisema hicho cha kwanza kwani kimebeba
mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu.
“Usomi
wowote unaendana na kusoma vitabu vya aina mbalimbali vikiwemo vya sayansi,
lugha na vyenginevyo, lakini Kuran ndio baba wa vitabu kwani hata hiyo sayansi
inapatikana humo na wavumbuzi wanaichota,” alieleza.
Kwa
hivyo, alisema Kuran ambayo haina mfano wake, inapaswa kufundishwa mtoto katika
umri mdogo lakini mafunzo hayo yaendane na kutekeleza kwa vitendo miongozo
yake.
Kwa
upande mwengine, Mwakilishi huyo amewashajiisha watoto na vijana kujitahidi
katika masomo, na kuwataka wasitumie mitandao kwa mambo yasiyofaa kimaadili,
bali waifanye kuwa ni kisima cha kuchota elimu yenye manufaa.
Mwakilishi
huyo alichangia mafeni sita kwa ajili ya zawadi kwa wanafunzi wanatakaofanya
vizuri zaidi kwenye mashindano hayo.
Hata
hivyo, aliwataka wanafunzi wa madrasa zinazoshiriki mashindano hayo, waepuke
kuhifadhi Kuran kwa tamaa ya zawadi, bali wafanye hivyo wakijua kitabu hicho
ndicho kitakachowaongoa na kuwapa manusura mbele ya Mwenyezi Mungu.
Simai
aliahidi kutoa kila aina ya msaada utakaohitajika ili kuyafanya mashindano hayo
yawe bora zaidi kwa faida ya watoto wa kanda ya Bungi na jimbo zima la Tunguu.
Mapema,
Katibu wa jumuiya ya Tahfidh Kkuran kanda ya Bungi Amir Juma Mussa Juma, aliwashukuru
wahisani waliochangia kufanikiwa kwa mashindano hayo kwa misaada waliyoitoa.
Alisema
michango wanayoitoa imesaidia kuyaimarisha licha ya changamoto kadhaa ambazo
wanajitahidi kuzitatua kila hali inavyoruhusu.
Alieleza
kuwa, wakati mashindano hayo yalipoanzishwa mwaka 1999 kwa kushirikisha wanafunzi
wa kike na kiume katika wanaohifadhi kuanzia juzuu tatu hadi 15, yameimarika
zaidi kwa kuongeza idadi ya washiriki kutoka 30 hadi zaidi ya 50.
IMETOLEWA
NA HABARI MAELEZO-ZANZIBAR
10
SEPTEMBA, 2018
No comments:
Post a Comment