Na
Abdi Shamnah
Wazanzibar wametakiwa kubadilika na kutumia ipasavyo vifaa vya kisasa vya ujenzi, ili
kuleta haiba ya nyumba zao, sambamba na kuishi maisha yalio bora.
Wito
huo umetolewa na Waziri wa Ardhi, nyumba, maji na nishati, Salama Aboud Talib katika
uzinduzi wa ‘show room ya Blossom Cheer, uliofanyika katika Hoteli ya Serena
Inn mjini hapa.
Show
room hiyo inayohusisha na uuzaji wa bidhaa ya mbao (milango) na Tiles, ni ya
kwanza kuanzishwa hapa Zanzibar, ikimilikiwa kwa ubia kati ya mwekezaji mzalendo
Seif Salum Zahor pamoja na raia wengine kutoka nchini China.
Alisema
ufunguzi wa show room hiyo ni fursa adhimu kwa Wazanzibari kupata bidhaa za
ujenzi zilizo bora na za bei nafuu, sambamba na kuondokana na usumbufu wa
kuagiza bidhaa hizo kutoka nchi za nje, hususan China.
“Uwepo
wake unaweza kubadili mfumo mzima wa maisha, husuan katika suala la makaazi kwa
kuwa na makaazi bora na yatakayoleta haiba katika mji wetu”, alisema.
Aliwataka
wamiliki wa kampuni za ujenzi hapa nchini kushirikiana na wamiliki wa show room
hiyo ili kuleta mabadiliko katika mfumo wa ujenzi kwa kuwa na majengo ya kisasa
na yenye vifaa vyote muhimu.
Aidha,
aliwaomba wawekezaji hao kuzingatia kwa makini hali za maisha ya wananchi na
kutimiza ahadi zao kwa kuingiza bidhaa bora, zenye viwango na zitakakavyopatikana
kwa bei nafuu ili wananachi waweze kuzimudu.
“Nawaomba
sana mzingatie sheria, kanuni na miongozo ya nchi yetu, hususan katika suala la
kulipa kodi ili kuwa na biashara isiyo na utata”, alisema.
Sambamba
na kuwataka biashara hiyo kuwa endelevu, aliwaomba kupanuwa wigo wa uingizaji
bidhaa kwa kuzingatia mahitaji ya Soko
la Utalii ambalo limeimarika sana hapa nchini, hususan katika ujenzi wa Hoteli
za kisasa.
Nae,
Meneja wa Show room hiyo Rocky Guo, alisema azma ya kufikisha huduma hizo hapa
Zanzibar ni kurahisisha upatikanaji wa
vifaa vya ujenzi kwa wananchi wa Zanzibar, kutoka kampuni kubwa ya uzalishaji
wa vifaa hivyo wanayoimiliki, ilioko jimbo la Guangzhou nchini China.
Alisema
pamoja na uingizaji wa vifaa hivyo, pia show room hiyo itajihusisha na shughuli
mbali mbali, ikiwemo kusarifu michoro ya ujenzi wa nyumba na majengo mbali
mbali, sambamba na kutowa ushauri na miongozo juu ya kupata bidhaa bora kutoka
nchini China na kuzifikisha nchini.
Alisema
tayari Kampuni yake ina matawi
(showroom) katika nchi zipatazo 20 Barani Afrika, ikiwemo nchi za Rwanda, Ethiopia,
Misri, Libya, Sudan, Benin, Cameroon na nyenginezo.
Mapema,
Mwekezaji mzalendo Zahor Salum, alisema wananchi na wakandarasi wa ujnezi
watakaonunua vifaa vitokanavyo na
mbao kutoka show room hiyo, watapatiwa
huduma za ufungaji katima majengo yao bila gharama zozote.
No comments:
Post a Comment