Naibu Waziri
wa Mambo ya Ndani
ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni, akiwaongoza Wajumbe
wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kilindi kuingia
Kituo cha Polisi cha Songe, ikiwa ni ziara ya kikazi ya Naibu Waziri kukagua shughuli za ulinzi na usalama wilayani
Kilindi mkoani Tanga
Naibu
Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza katika kikao cha ndani
kilichohusisha Wajumbe wa
Kamati ya Ulinzi
na Usalama ya
Wilaya ya Kilindi ikiwa
ni ziara ya kikazi
ya Naibu Waziri
kukagua shughuli za
ulinzi na usalama
wilayani Kilindi mkoani Tanga . Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya
Kilindi, Sauda Mtondoo na Kulia ni Katibu
Tawala wa Wilaya
hiyo, Warda Abeid.
Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Sauda Mtondoo akizungumza katika kikao cha ndani
kilichohusisha Wajumbe wa
Kamati ya Ulinzi
na Usalama ya
Wilaya ya Kilindi ikiwa
ni ziara ya kikazi
ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni
(katikati) kukagua shughuli za
ulinzi na usalama
wilayani Kilindi mkoani Tanga . Kulia ni Katibu
Tawala wa Wilaya
hiyo, Warda Abeid.
Kamanda wa Polisi Mkoa
wa Tanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi , Edward Bukombe, akizungumza katika
kikao cha ndani kilichohusisha
Wajumbe wa Kamati
ya Ulinzi na
Usalama ya Wilaya
ya Kilindi ikiwa ni ziara
ya kikazi ya
Naibu Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani, ) kukagua shughuli
za ulinzi na
usalama wilayani Kilindi
mkoani Tanga.
Picha
na Wizara ya Mambo
ya Ndani ya
Nchi
Na Mwandishi Wetu
Serikali imedhamiria kujenga
Vituo vya Polisi 65 katika wilaya mbalimbali nchini ikiwa ni juhudi za
kukabiliana na uchakavu na upungufu wa
vituo vya polisi nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni baada ya kutembelea na
kukagua Kituo cha Polisi cha Songe ambacho ndio kituo kikuu katika Wilaya ya
Kilindi mkoani Tanga
Alisema Serikali
inatambua changamoto za vituo vya polisi ikiwemo uchakavu, udogo wa majengo
katika vituo mbalimbali nchini na iko katika mpango wa kujenga vituo vya polisi
65 ili kuwepo na ulinzi thabiti wa raia na mali zao.
“Serikali inatambua
changamoto ya vituo vya polisi hasa katika wilaya mpya nchini, ikiwepo uchakavu
wa majengo, kwahiyo uko mkakati maalumu wa kujenga vituo vya polisi 65 nchi
nzima ili kuweza kukabiliana na matukio ya kiuhalifu, lengo la serikali ni
kuhakikisha raia wake na mali zao zinakua salama na matukio ya kiuhalifu
yanapungua na kutoweka kabisa,” alisema Masauni
Alisema Serikali pia
inakaribisha nguvu za wananchi na wadau mbalimbali ambao wako tayari kusaidia
ujenzi wa vituo vya polisi huku akipongeza baadhi ya maeneo nchini ambako vituo
vya polisi vimejengwa kwa ushirikiano wa michango ya wananchi na serikali.
Awali akitoa taarifa ya
Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kilindi,
Mkuu wa Wilaya ya Kilindi na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Sauda
Mtondoo alisema hali ya uhalifu kuanzia kipindi cha Januari hadi Oktoba 2018
ilikua ya wastani huku kukiripotiwa upungufu wa makosa kwa asilimia 9.8 kati ya
mwaka 2018 na 2017.
“Kwa mujibu wa takwimu
za uhalifu kulikuwa na jumla ya makosa makubwa ya jinai 163 ndani ya mwaka huu
yaliyoripotiwa kwa kulinganisha na makosa 179 yaliyoripotiwa ndani ya mwaka
2017, ukiwepo upungufu wa makosa 16 katika vipindi hivyo viwili,” alisema Sauda
Akizungumza wakati wa
ziara hiyo, Mbunge wa Kilindi, Omari Kibua alimshukuru Naibu Waziri kwa kufika jimboni hapo kujionea
hali halisi ya kituo hicho kikuu cha wilaya baada ya kumuomba kufanya hivyo wakati wa kikao cha bunge
kilichomalizika hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment