Habari za Punde

Serikali Kufikisha Umeme Nanyamba Mkoani Mtwara Kabla ya Sherehe za Mwaka Mpya 2019 - Dkt.Kalemani.

Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Kilimanjaro katika wilaya ya Nanyumbu
 Mbunge wa Jimbo la Nanyamba Abasi Chikota akizungumza na wananchi
 MKUU wa wilaya ya Nanyamba Evod Mmanda akizungumza
 Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani katika akitazama nguzo
 Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nishati Dkt Kalemani
Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani amesema dhamira yake ni kuhakikisha huduma ya umeme  inafika katika wilaya ya Nanyamba mkoani Mtwara kwenye maeneo mengi kabla ya Sherehe za mwaka mpya wa 2019 ili kuweza kutoa fursa ya wananchi kunufaika na huduma hiyo muhimu kwa maendeleo.


Dkt Kalemani aliyasema hayo kwenye  mtaa Kilimanjaro wilaya ya Nanyamba mkoani Mtwara wakati wa ziara yake ambapo alisema  haridhishwi na kasi ya mkandarasi aliyepewa kazi ya kuunganisha vijiji vya Nanyamba na kusema kuwa anatoa siku 20 kwa mkandarasi huyo kukamilisha kazi ya kuunganisha umeme mtaa wa kilimanjaro na maeneo ya jiran hasa kwenye taasisi zinazohudumia jamii kama hospitali na shule.

“Sijaridhishwa na kasi ya mkandarasi, Sasa leo wakati sisi tunaondoka mkandarasi yeye atabaki, ili kuhakikisha kabla ya sikukuu ya chrismas na mwaka mpya umeme Nanyamba unawaka, mkandarasi aweke magenge yake hapa nataka kazi ifanyike”

Aidha waziri Dkt.Kalemani amelitaka Shirika la Umeme Tanzania,TANESCO kufungua ofisi katika wilaya ya Nanyamba ili kusogeza huduma kwa wananchi, ambao wapo tayari kulipia huduma ya Umeme

“Wanamtwara wote ninaimani uwezo wa kulipa ela ya kuunganishiwa umeme mnayo, hasa kipindi hiki ambacho Serikali inanunua mazao ya korosho hapa mtwara, hivo naamini wote hapa kwa Sasa uwezo wa kulipia elfu 27ya umeme mnao"Alisema

Alieleza kutokana na hali hiyo Shirika hilo litafungua ofisi yao Nanyamba ili kusudi waweze kulipia na kuongeza kuwa vifaa maalum vya Umeme Tayari (UMETA) 250 vitatolewa kwa wananchi ambao hawana uwezo wa kutandaza nyaya katika nyumba zao ili waweze kuunganishwa na huduma ya Umeme.

Waziri wa Nishati Dkt.Medard kalemani yupo mkoani Mtwara, akifanya ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya Miradi ya Umeme vijijini (REA)na kuwataka wananchi kuutumia umeme kama fursa ya kujiongeZea kipato kupitia biashara mbalimbali

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.