Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wanachama wa CCM Wilaya ya Mkoani Pemba, katika Ukumbi wa Skuli ya Mohammed Juma Pindua, Mkoani akiwa katika ziara yake Kisiwani Pemba.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein ambaye pia ni Makamu
Mwenyekiti wa CCM Zanzibar amesema kuwa siasa za vyama vingi zimekuja kwa lengo
la kushidana kwa Sera na sio kukashifiana.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo wakati akizungumza na viongozi wa CCM wa Wilaya ya Mkoani Pemba
pamoja na kufanya Majumuisho ya ziara yake kwa Wilaya hiyo, yaliyofanyika
katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari ya Mohamed Juma Pindua, iliyopo Mkanyageni
Mkoa wa Kusini Pemba ambapo viongozi kadhaa walihudhuria akiwemo Mke wa Rais wa
Zanzibar Mama Mwanamwema Shein.
Katika hotuba yake Makamu
Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Rais Dk. Shein alisema kuwa siasa za vyama vingi
havikuja kwa lengo baya la kukashifana na badala yake lina lengo zuri la
kushindana kwa Sera ili iwe kivutio kwa wanachama na sio ugomvi.
Hivyo, Rais Dk. Shein
aliwasisitiza wananchi wa Wilaya hiyo kuishi kwa mapenzi na kufahamiana
sambamba na kushirikiana pamoja kwao wote ni ndugu.
Aidha, Makamu huyo
Mwenyekiti wa CCM Zanzibar aliwataka viongozi wa CCM kutembelea Matawi, Wadi,
Majimbo na Wilaya zao sambamba kuwatembelea wananchi na wanachama wa chama chao
ili kuwasikiliza changamoto walizonazo na kuzitafutia ufumbuzi.
Pia, Rais Dk. Shein
aliwataka viongozi wa CCM wa Wilaya hiyo kuimarisha miradi ya ili chama hicho
kiweze kupata mapato ya kuweza kukiimarisha na kuapata mafanikio makubwa zaidi.
Rais Dk. Shein
alieleza kuwa tayari utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015-2020
imeshatekelezwa kwa kiasi kikubwa na ahadi nyingi zilizoahidiwa
zimeshatekelezwa sambamba na zile ambazo haziko katika Ilani.
Alisisitiza kuwa
viongozi wote waliomo Serikalini ni vyema wakatambua kuwa wanatekeleza Ilani ya
Uchaguzi ya Chama cha CCM, hivyo, wanakila sababu kufanya kazi zao kwa bidii na
yule ambaye hatoweza anapaswa kukaa pembeni.
Aliongeza kwua huo ni
utaratibu wa Serikali zote duniani kwa chama kinachoongoza Serikali ni lazima viongozi wote watekeleze Ilani ya
Chama hicho kwani ndicho kilicho madarakani na ndicho kinachoongoza nchi.
Rais Dk. Shein
alieleza kuwa huo ndio utaratibu wa kimataifa na demokrasia ya nchi hivyo
viongozi wote waliomadarakani katika Serikali anayoiongoza hawana budi
kutekeleza Ilani ya CCM kwani ndicho chama kilicho madarakani,
Alieleza kuwa ujenzi
wa barabara ya Mkanyageni- Kangani (Km
6.5) ni moja ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 ambayo
imetajwa katika Ilani hiyo kwenye ukurasa wa 149.
Aidha, ujenzi wa jengo
la skuli ya Sekondari Michenzani, Mkoani Pemba pia ni utekelezaji wa Ilani ya
uchaguzi katika kuimarisha sekta ya elimu Zanzibar.
Ambapo pia, Rais Dk.
Shein alieleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya CCM ya
kujenga barabara ya Chake hadi Mkoani yenye (Km 27), ambayo hivi sasa imo
katika mchakato wa michoro.
Rais Dk. Shein pia,
aliusisitiza uongozi wa CCM wa Mkoa na Wilaya hiyo kuimarisha historia ya ASP
kwa kulijenga jengo la Tawi la CCM lenye historia ya ASP huko Mkanyageni ambalo
lilitumika na wazee waasisi kama vile marehemu mzee Mohamed Juma Pindua na yeye
kuahidi kuchangia mabati kwa ajili ya ujenzi huo.
Sambamba na hayo, Rais
Dk. Shein alizipongeza taarifa zilizotolewa mbele yake ikiwemo taarifa ya
Serikali ya Wilaya ya Mkoani pamoja na taarifa ya Chama iliyotolewa na uongozi
wa CCM Wilaya ya Mkoano.
Rais Dk. Shein pia,
aliupongeza uongozi wa CCM Wilaya hiyo ya Mkoani kwa kuongeza idadi ya
wanachama sambamba na ulipaji wa ada kwa wanachama wa chama hicho.
Rajab
Mkasaba, Ikulu
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment