Habari za Punde

WAZIRI MHAGAMA AKAGUA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MKOANI SONGWE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Viongozi na watendaji wa Mkoa wa Songwe mara baada ya kuwasili Mkoani hapo wakati wa ziara yake ya kukagua maandalizi hayo Mkoani humo. (Kushoto) ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza. 
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela akitoa taarifa ya Mkoa wa Songwe kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipowasili mkoani humo kukagua maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipitia kwa makini ripoti ya maandalizi ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru alipowasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe kupokea taarifa hiyo. (Kulia) ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Songwe Bw. Elinico Mkola.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo mara baada ya kupokea taarifa ya maandalizi alipofanya kikao kifupi na baadhi ya Wanakamati ya Maandalizi ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Songwe. (Kushoto) ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza na Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela. (Kulia) ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Songwe Bw. Elinico Mkola.
Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Songwe wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kuhusu maandalizi ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Vijana wa Halaiki wakitengeneza umbo la Mlima Kilimanjaro kuashiria kupandisha Bendera ya Taifa katika mlima Kilimanjaro wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipotembea vijana hao katika shule ya msingi ya Ichenjezya ambapo vijana hao wa halaiki wanafanya maandalizi.
Vijana wa Halaiki wakitengeneza umbo la Mlima Kilimanjaro kuashiria kupandisha Bendera ya Taifa katika mlima Kilimanjaro wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipotembea vijana hao katika shule ya msingi ya Ichenjezya ambapo vijana hao wa halaiki wanafanya maandalizi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akitoa maelezo kwa walimu wa halaiki mara baada ya kukagua na kujionea hatua za awali za maandalizi ya vijana wa halaiki.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Bw. James Kajugusi (wa pili kutoka kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alipotembea Uwanja wa Mlowo kujionea hali ya maandalizi. (Kushoto) ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza.
Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi, Mhandisi Tanu Deule akitoa maelezo kuhusu Uwanja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (watano kutoka kushoto) alipotembelea na kukagua hali ya Uwanja na miundombinu mbalimbali katika uwanja wa Mlowo zitakapofanyika Sherehe hizo(mwenye miwani) ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela. (Wa tatu kutoka kushoto) ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza.
PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU
(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

Na; OWM (KVAU) - Songwe
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amefanya ziara na kukagua maandalizi ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru zinazotarajiwa kufanyika tarehe 2 Aprili, 2019 Mkoani Songwe.
Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwenye kamati ya Maandalizi, Waziri Mhagama alieleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi na kuipongeza kamati ya Mkoa kwa kusimamia vyema na kuratibu shughuli za maandalizi hayo.
“Niwapongeze kwa hatua hizi mlizofikia katika kuhakikisha shughuli hii ya kitaifa inafana, maana maandalizi bora yataleta heshima kwa Mkoa katika kufanikisha jukumu hilo muhimu, hivyo mzingatie masuala yote ya msingi na kufanya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Songwe una kuwa wa kihistoria,” alisema Waziri Mhagama
Aliongeza kuwa, Mbio za Mwenge wa Uhuru zinahistoria kubwa katika Taifa letu, ikiwa ni mwaka wa 55 sasa tunaadhimisha mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa na ni mwaka wa 27 toka kuanzishwa mfumo wa vyama vingi ikiwa ni kielelezo tosha cha kukua kwa demokrasia nchini.
Vilevile ni miaka 20 ya kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere hivyo ni vyema vijana wakatambua historia ya Taifa na kujifunza falsafa za Baba wa Taifa kwa kuwa na umoja, mshikamano, uzalendo, kujitolea na zaidi kuchochea maendeleo ya nchi.  
“Kupitia shughuli hii ya kitaifa vijana wanapaswa kutumia fursa hiyo kuelewa historia ya Taifa lao pamoja na Mwenge wa Uhuru kama kielelezo muhimu cha Utaifa,” alisisitiza Mhagama  
Hata hivyo, Mhe. Mhagama aliusihi uongozi wa Mkoa kutumia nafasi hiyo kutangaza vivutio vya utalii, fursa za kiuchumi na shughuli mbalimbali zilizopo ndani ya mkoa wa Songwe. Pia aliwataka waendelee kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uzinduzi.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela, alipokea maelezo yaliyotolewa na kuahidi kusimamia shughuli zote za maandalizi kwa ufanisi na kukamilisha ndani ya muda uliopangwa.
“Nikuhakikishie maandalizi yataendelea kwa kasi na yatakamilika kwa wakati ili kuwawezesha wananchi wa Mkoa wa Songwe wanashiriki katika tukio hilo muhimu na kuitumia fursa hiyo ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kujitangaza kama Mkoa,” alisisitiza Mhe. Mwangela

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.