MWAKILISHI wa Shirika la Wafanyakazi Duniani ILO Bi. Getrude Sima
akitowa Salama za ILO wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
iliofanyika katika Ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein, SUZA Tunguu Wilaya ya Kati
Unguja
Mwenyekiti wa
Shirikisho la Vyama vya Wafanyaazi,
Ndugu Ally Mwalim Rashid
Makamu wa
Pili wa Rasi wa Zanzibar, Mheshimiwa
Balozi Seif Ali Iddi.
Waziri wa
Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto,
Mheshimiwa Mama Moudline Syrous Castico.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Jumuiya ya Wafanyakzai (ZANEMA), Ndugu Abdallah Salah Salim Salah.
Mkuu wa Mkoa
wa Kusini Unguja, Mheshimiwa Hassan Khatibu Hassan
Waheshimiwa
Mawaziri, Wawakilishi, Wabunge na Viongozi wengine wa serikali mliopo
Viongozi wote
mliopo meza kuu na meza jirani na meza kuu,
Katibu Mkuu
Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Zanzibar – ndugu Khamis Mohamed
Viongozi wa
vyama vya wafanyakazi, ndugu wafanyakazi, Ndugu waalikwa na wananchi
mliohudhuria
Ndugu
waandishi wa Habari.
Itifaki
inazingatiwa.
ASALAAM
ALAYKUM,Heri ya sikukuu ya Mei Mosi 2019
Ni furaha na heshima kubwa kwangu kuwepo hapa nanyi leo ili kusherekea
siku hii kubwa ya wafanyakazi ulimwenguni kote yenye kubeba dhima isemayo”Kuimarika kwa Uchumi wa Taifa Kuendane na
kuongezeka kwa maslahi ya wafanyakazi“.
Ni siku iliyo
na historia kubwa na inayo-ashiria umoja wa wafanyakazi na kuhimiza kuwepo
mazingira staha ya kazi.
Umuhimu wa siku
hii unajionyesha pia Zaidi wakati Shirika la Kazi Duniani likiadhimisha miaka mia
moja mwaka huu.
Mheshimiwa mgeni rasmi na wageni waalikwa,
Shirika la
Kazi Duniani lilianzishwa miaka mia moja iliyopita wakati wa mageuzi
yaliyotokana na vita ya kwanza ya Dunia. Wafanyakazi walidai haki sawa na
kuheshimiwa kazini, mishahara ya kutosha, masaa nane ya kazi kwa siku na uhuru
wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi. Kwenye Katiba ya Shirika la Kazi Duniani
maneno ya mwanzo yanasema – “Amani ya
kudumu ulimwenguni inaweza kuwepo tu endapo kuna haki ya Kijamii”
Muundo wa ILO
wa Utatu ndio chanzo cha uimara na ushirikiano.
Wafanyakazi, Waajiri na Serikali hufanya kazi kwa pamoja kupitia misingi
ya majadiliano ya Pamoja na kufikia muafaka.
Mheshimiwa mgeni rasmi na wageni waalikwa,
Shirika la Kazi Duniani linafurahishwa na ushirikishwaji wake kwenye
malengo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuiendeleza nchi kufikia uchumi
wa kati ifikapo mwaka 2020 na kuboresha maisha na ustawi wa watu wa Zanzibar. Mkakati
wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar wa miaka mitano umeonyesha
wazi jinsi Serikali itakavyofikia lengo hili.
Hili
linatukumbusha kuzingatia kuwa wafanyakazi ni nguzo katika maendeleo na ustawi
wa jamii. Wapo mstari wa mbele katika mikakati ya maendeleo na ni vizuri
kuyatambua majukumu yao hasa katika – kupatiwa maslahi na mazingira mazuri ya
kazi. Wakati tukiangalia kuhusu kazi za Shirika la Kazi Duniani kwa miaka 100
iliyopita, ni vema pia kuangalia mustakabali wa kazi zake, hasa ukizingatia
mabadiliko yanayoendelea kutokea kwenye ulimwengu wa kazi. Ripoti ya Kamisheni
ya ILO kuhusu Mustakabali wa Kazi, iliyozinduliwa tarehe 22 Januari mwaka huu, inapendekeza
kuwepo kwa mfumo wa maendeleo unaolenga maendeleo ya watu katika Mustakabali wa
kazi sambamba na kuzingatia kazi zenye staha, kuondokana na umasikini kwa
kuendeleza maendeleo ya watu, será za kijamii na ukuaji wa uchumi.
Mheshimiwa mgeni rasmi na wageni waalikwa,
Shirika la
Kazi Duniani (ILO) linaendelea kufanya kazi na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar pamoja na vyama vya wafanyakazi na waajiri nchini katika kuendeleza
ajenda ya Kazi zenye Staha kupitia yafuatayo:
§
Kuendeleza
ajira kwa kukuza ujuzi kwa njia ya mafunzo yanayotolewa kwa kushirikiana na
taasisi ya mafunzo na waajiri katika sekta ya utalii.
§
Sera ya
hifadhi ya jamii
§
Programu
ya pamoja ya mashirika ya umoja wa mataifa kwa Zanzibar
§
Kuimarisha
uwezo wa kamati za utatu kushiriki kwenye majadiliano ya utatu
Mheshimiwa Raisi, Shirika la kazi Duniani linatambua na kupongeza
juhudi za serikali yako kupitia sera ya Uchumi wa Viwanda kwani italeta fursa
nyingi za ajira kwa vijana wa Zanzibar.
Mheshimiwa mgeni rasmi na wageni waalikwa,
Kama ILO
tutaendelea kuunga mkono juhudi za serikali, vyama vya wafanyakazi na waajiri
katika kukuza ajira zenye staha ili kuimarisha maisha ya watu wa Zanzibar na
hasa wafanyakazi.
Asanteni sana
kwa kunisikiliza, na nawatakia sikukuu njema!!
No comments:
Post a Comment