MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM)
Mkoani Tanga Omari Mwanga kulia akiwa kwenye msiba huo katikati ni
Katibu wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo kushoto ni Katibu wa
Hamasa na Chipukizi wa (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM)
Mkoani Tanga Omari Mwanga kulia akiwa kwenye msiba huo katikati ni
Katibu wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo kushoto ni Katibu wa
Hamasa na Chipukizi wa (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed
Sehemu ya Viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga wakiwa msibani leo
Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed
akifuatilia matukio mbalimbali kwenye msiba ambapo aliyefariki alikuwa
akifanya naye kazi.
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM)
Mkoani Tanga Omari Mwanga leo amewaongoza viongozi mbalimbali wa jumuiya
kwenye mazishi ya aliyekuwa Katibu wa Hamasa na Chipukizi (UVCCM) Kata
ya Chumbageni Jijini Tanga Marry Dominic Dawa yaliyofanyika Bombani
Muheza.
Kabla ya mwili huo kusafirishwa kuelekea wilayani Muheza aliagwa eneo la
Kange Kasera Jijini Tanga ambapo Jumuiya ya Umoja wa Vijana mkoa wa
Tanga walitoa salamu zao wakati wa halfa hiyo
Akizungumza wakati kuagwa mwili huo Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tanga
Mwanga aliwapa pole wafiwa na kuwataka kuwa wavumilivu kwenye kipindi
hicho kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.
Alisema wao kama Jumuiya wapo pamoja na familia kwenye kipindi hicho
kigumu huku wakimuelezea namna katibu huyo alivyokuwa mchapakazi na
hodari katika utendaji wake.
Kwa kweli hapa tumepata pigo kubwa hasa ukizungatia Marry alikuwa
kiongozi hodari na shupavu kwenye kuwajibika kwenye nafasi aliyokuwepo
huku wakieleza mchango wake utaendelea kukumbukwa.
Hata hivyo aliwataka viongozi waliobakia kuiga mazuri yaliyofanywa na
kiongozi huyo katika kuhakikisha Jumuiya hiyo inapata mafanikio makubwa .
Msiba huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu wa UVCCM
Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo,Katibu wa (UVCCM) wilaya ya Tanga Fahad
Siraji,Katibu Hamasa wilaya ya Tanga (UVCCM) Kipanga Juma,Mjumbe wa
Baraza Taifa (UVCCM) Mbaruku Asilia.
Imetolewa na Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Mkoa wa Tanga Katibu wa Hamasa na Chipukizi (UVCCM) Mkoa wa Tanga
No comments:
Post a Comment