Mkuu wa Wilaya ya
Uyui mkoani Tabora mhe. Gift Msuya akifungua mafunzo kwa wakulima wa Kata
ya Miyenze Wilayani humo hivi karibuni,mafunzo hayo yakuwajengea uwezo wakulima
waliorasimisha mashamba yao Wilayani humo na kupatiwa hati za haki milki za
kimila za kumilki ardhi yamefanyika katika Kata za Miyenze na Lutende.
Meneja Urasimishaji
Ardhi Vijijini kutoka MKURABITA Bw. Antony Temu akisisitiza kuhusu umuhimu wa
mafunzo yakuwajengea uwezo wakulima waliorasimisha mashamba yao Wilayani Uyui
na kupatiwa hati za haki milki za kimila za kumilki ardhi.
Sehemu ya wakulima walioshiriki mafunzo yakuwajengea uwezo ili waweze kutumia hati milki za kimila za kumiliki ardhi ili kujiletea maendeleo wakifuatilia mafunzo hayo hivi karibuni katika Kata ya Miyenze.
Mkuu wa Wilaya ya
Uyui mkoani Tabora mhe. Gift Msuya akiwa kwenye picha ya pamoja na
wananchi waliopatiwa hati za haki milki za kimila za kumiki ardhi Wilayani humo hivi karibuni wakati wa hafla
ya kufungua mafunzo hayo yaliyowanufaisha wakulima zaidi ya 200 katika Wilaya
hiyo ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kuwakwamua kiuchumi wakulima hapa
nchini.
Wananchi Wilayani Uyui Mkoani Tabora Wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John
Pombe. Magufuli. kwa kuwawezesha kurasimisha mashamba yao na kupatiwa hati za hakimilki za kumiliki ardhi hali inayowawezesha kujikwamua kiuchumi.
Baadhi ya wananchi hao wakizungumza wakati wa mahojiano maalum Wilayani humo akiwemo mkazi wa Miyenze Bw.
Julius
Magoi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imeonesha dhamira ya dhati kuwawezesha wananchi Vijijini kupitia Mpango wa Kurasimishaji Rasilimali na Biashara za Wanyonge
Tanzania (MKURABITA).
“Tunamshukuru Rais Dkt.Magufuli kwa kuwezesha MKURABITA kuturasimishia mashamba yetu,
kuyapima na kupatiwa hati za hakimilki za kimila hali inayotuwezesha kuongeza tija katika uzalishaji mashamba ni hasa katika mazao ya biashara”
Alisisitiza Bw. Magoi.
Akifafanua amesema kuwa
MKURABITA imeendesha mafunzo yanawawezesha wakulima kuendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano kuwakwamua wananchi wanyonge hasa wanaoishi vijijini katika Wilaya hiyo kwa kuwajengea stadi za kilimo
bora, ufugaji wa kuku kibiashara, kilimo cha pamba, alizeti na mazao mengine.
Kwa upande wake mkazi mwingine wa
Kata hiyo
Bi.Nyamizi Shija amesema kuwa anamuomba Rais.Dkt.Magufuli aendelee na jitihada zake za kuwawezesha wananchi kama ambavyo anafanya sasa kwa kuwa wanaendelea kumuunga mkono katika kila jambo analofanya ili kuwaletea maendeleo.
Aliongeza kuwa utendaji mzuri wa Serikali ya Awamu ya Tano umewawezesha wananchi kunufaika na rasilimali za nchi yao ikiwemo kutolewa kwa fedha zinzoelekezwa Vijijini kuwajengea uwezo akitolea mfano urasimishaji wa ardhi ambayo ni nyenzo kuu ya kuwawezesha wananchi.
Naye mkazi wa Kata
ya Lutende Bw. Omari Mohamed amesema kuwa Serikali imeonesha kuwajali, kuwatambua,
kuwathamini na kuwawezesha wananchi vijijini kwa kuwa inachukua hatua kuimarisha sekta zenye kuwainua wananchi ikiwemo kilimo na mifugo hali itakayowezesha kufikiwa kwa malengo ya kutukwamua kiuchumi kama wakulima.
“Rais Magufuli yuko makini,
anatetea wanyonge na anaelewa mahitaji ya wananchi tunaoishi vijijini ndio maana tumepata fursa ya kujengewa uwezo kupitia
MKURABITA
na kurasimishiwa mashamba yetu hali iliyotuwezesha kupata hati za hakimilki za kimila za kumiliki ardhi ambazo tutazitumia kujikwamua kiuchumi”
Alisisitiza Mohamed
Akifafanua Mohamed
amesema kuwa wananchi wanaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuwaletea maendeleo.
Kwa upande wake
Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini kutoka MKURABITA Bw. Antony Temu amebainisha kuwa wananchi wa
Kata za Miyenze na Lutendewa mejengewa uwezo wa kutekeleza kilimo chenye tija cha
mazao ya biashara kama alizeti, pamba na mengine ili waweze kuzalisha kwa tija.
Aliongeza kuwa mada nyingine walizofundishwa wakulima hao ni pamoja na utunzaji wa mazingira,
utunzaji wa kumbukumbu, fursa zilizopo katika taasisi za fedha, uandaaji wa mpango wa biashara na uanzishaji wa vyama vya ushirika.
Mafunzo ya kuwajengea uwezo wananchi waliorasimisha mashamba yao na kupatiwa hati za hakimilki za kimila yamefanyika katika
Kata ya Miyenze na Lutende Wilayani Uyui mkoani Tabora na kushirikisha wakulima zaidi ya
200.
No comments:
Post a Comment