STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Dar es Salaam 18.08.2019

RAIS wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amefunga mkutano wa Wakuu wa Nchi
na Serikali za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na kutoa pongezi
zake kwa heshima iliyopewa Tanzania kufuatia lugha ya Kiswahili kuteuliwa kuwa lugha
ya nne itakayotumiwa rasmi katika Jumuiya hiyo.
Hafla
hiyo imefanyika leo katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi hizo za (SADC)
uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini
Dar-es-Salaam uliohudhuriwa na viongozi
mbali mbali wa nchi za Jumuiya hiyo ya (SADC) akiwemo Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.
Katika
hotuba yake hiyo, Rais Magufuli alieleza kuwa kukifanya Kiwashili kuwa ni lugha
rasmi ya Jumuiya hiyo ni heshima kubwa hasa kwa muasisi wa Taifa hili Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere na kusisitiza kuwa kiongozi huyo alikuwa na upendo kwa
watu na alijitolea kutoa upendo wake sio tu kwa Watanzania bali hata wananchi
wa nchi jirani na Afrika kwa jumla.
Alieleza
kuwa Tanzania imekuwa ikifanya juhudi kubwa katika kuhakikisha amani na utulivu
inapatikana kwa nchi za Bara la Afrika. Juhudi hizi ni kuendeleza historia
kubwa ambayo iliyoanza wakati wa harakati za ukombozi ambapo katika harakati
hizo
lugha ya Kiswahili ilitumika na ilikwa na mchango
mkubwa katika kuwaunganisha
wanaharakati wa nchi mbali mbali
Akitolea
mfano, Rais Magufuli alisema kuwa mnamo mwaka 1975 Jeshi la wananchi Tanzania
(JWTZ) lilikwenda nchini Shelisheli kuzima Mapinduzi pamoja na nchi nyengine
kadhaa za Bara la Afrika.
Alieleza
kuwa kutumika kwa lugha ya Kiswahili katika Jumuiya hiyo imepelekea Watanzania kufurahishwa
na hatua hiyo na kuwapongeza wakuu wa nchi za (SADC) kwa kukuza na kuendelea
historia hiyo ya kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya nne katika Jumuiya hiyo.
Alisisitiza
kuwa hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza ushirikiano na utengamano wa
wananchi “Kiswahili ni lugha ya Afrika na sisi ni wananchi wa Bara hilo hivyo
tunapaswa kuitumia lugha ya Kiswahili”, aliongeza Dk. Magufuli.
Rais
Magufuli alitumia fursa hiyo kuwataka viongozi wa nchi za (SADC) kuiga mfano wa
nchi ya Afrika ya Kusini ambayo kuanzia mwakani itaanza kufundisha Kiswahili
katika Skuli zake na kuongeza kuwa Tanzania iko tayari kusaidia kufanikisha malengo
ya Taifa hilo la kufundisha na kutumia Kiswahili katika shughuli mbali mbali.
Aidha,
Rais Magufuli alieleza kuwa mkutano huo wa siku mbili umekuwa wa mafanikio
makubwa sana na kuweza kufanyika kwa upendo mkubwa huku akieleza kuwa viongozi
wakuu wa nchi za (SADC) walijadiliana kwa umakini mkubwa na hatimae kufikia
makubaliano ambapo ajenda nyingi zilijadiliwa na kufikia maamuzi.
Akieleza
jinsi nchi za Jumuiya hiyo zilivyoshindwa kufikia kukua kiuchumi kwa asilimia
saba na badala yake zilikuwa kwa asilimia tatu hivyo Rais Magufuli alisisitiza
haja ya kuimarisha Sera za uchumi na fedha kwa nchi hizo.
Pamoja
na hayo, alieleza kuwa ombi la Burundi la kujiunga na Jumuiya hiyo pamoja na
suala la Zimbwabwe yalizungumzwa na kufikiwa muwafaka mzuri ambapo nchi zote
wanachama zimeunga mkono nchi ya Zimbabwe kuondolewa vikwazo huku kwa upande wa
Burundi imepewa muda zaidi kukamilisha baadhi ya mambo.
Rais
Magufuli pia, alitumia fursa hiyo kueleza jinsi Itifaki zilizosainiwa katika
mkutano huo wa leo na kusema kuwa hatua hiyo ni miongoni mwa mikakati ya
kuhakikisha maamuzi yanatekelezwa kwa haraka zaidi.
Aliipongeza
ripoti ya Mwenyekiti anaemaliza muda wake pamoja na ripoti ya Sektarieti kwa
kuwa zimebainisha wazi kazi nzuri iliyofanywa na viongozi hao katika kipindi
chote cha uongozi wao. Aidha, alitoa pongezi kwa washirika wa maendeleo na taasisi mbali mbali za Kimataifa zinauna mkono na kufanya kazi kwa karibu na Jumuiya
ya (SADC).
Nae
Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi alitoa nene la shukurani katika mkutano huo, ambapo alitoa a pogezi kwa mashirikiano
yaliopo katika Jumuiya hiyo na kutoa pongezi maalum kwa Rais Magufuli kwa
Tanzania na wananchi wa Tanzania kwa kufanikisha mkutano huu na ukarimu mkubwa
walionyesha kwa wageni waliofika nchini.
Sambamba
na hayo, alitumia fursa hiyo kutoa
shukurani kwa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Wananchi kwa misaada mbali mbali waliyotoa kwa
ndugu
zao wa Msumbiji wakati walipopata janga la kimbunga na mafuriko nchini humo.
Vile
vile, alitumia fursa hiyo kuwakaribisha
viongozi wote wa (SADC) katika Mkutano wa 40 utakaofanyika nchini Msumbiji
mwaka 2020 ambapo Rais wa nchi hiyo atakabidhiwa
kijiti cha Uwenyekiti wa (SADC).
Mapema
zoezi la kutiwa saini kwa Itifaki na
viongozi wan chi za Jumuiya hiyo lilifanyika.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment