Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akihutubia wakati akilifungua Kongamano la Wajasiriamali Wanawake Zanzibar linalofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu (SUZA) kulia Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar.Mhe. Maudline Castico na kushoto Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa.Bi.Thuwaiba Editon Kisasi, ufunguzi huo umefanyika leo.19-10-2019.
MKE wa Rais wa Zanzibar, mama Mwanamwema Shein
amesema shughuli za ujasiriamali zinahitaji taaluma ili ziweze kufanyika kwa
ufanisi na kuleta tija pamoja na kuondokana na changamoto.
Mama Mwanamwema amesema
hayo katika ufunguzi wa Kongamano la
Wajasiriamali wanawake wa Mikoa ya Unguja, hafla iliyofanyika katika
Ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein, SUZA - Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja.
Alisema shughuli za
ujasiriamali kama ilivyo shughuli nyengine zinahitaji elimu ya nadharia na
vitendo ili kumwezesha mjasiriamali kupata tija na kuongeza kipato katika
familia,
Alisema kwa kuelewa
umuhimu wa shughuli za ujasiriamali kwa wananchi, Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Awamu ya saba inayoongozwa na Rais Dk. Shein imeunda Wizara ya Kazi,
Uwezeshaji, Wazee, wanawake na watoto, pamoja na kaunzisha Mfuko wa Uwezeshaji
wa wananchi kiuchumi ili kufanikisha azma hiyo.
Alieleza kuwa Serikali
imeandaa mipango mbali mbali ya kuwasaidia wananchi ili kuongeza kipato, hivyo
akawataka wananchi kuzitumia ipasavyo fursa zilizopo ili kuongeza kipato cha
familia.
Aidha, Mama Mwanamwema
alipongeza Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), kw uamuzi wa kuandaa kongamano
hilo, ambapo pamoja na mambo mengine linazungumzia umuhimu wa kuimarisha
Daftari la wapiga kura.
Alisema wakati huu
wananchama wa CCM wakiajiandaa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao mwakani, kuna
umuhimu wa kukumbushana haja ya kuimarisha daftari la kudumu la wapiga kura,
hivyo akatowa wito kwa kila mmoja kushiriki na kutekeleza wajibu wake wakati
utakapofika.
Alisema ili kufanikisha
azma ya kuipatia ushindi CCM, ni muhimu kila mmoja kushiriki katika uimarishaji
wa daftari hilo, kwa msingi kuwa bila ya kujiandikisha hakutakuwa na fursa ya
mtu kupiga kura.
Aliwakumbusha washiriki
wa kongamano hilo kuwa CCM ndio chama kinachotegemewa na Watanzania katika
kuwaletea maendeleo, kudumisha amani na umoja, kulinda Mapinduzi pamoja na
kudumisha Muungano, hivyo kuna kila sababu ya kukiandalia mazingira bora ya ushindi.
“Tusisahau kuwa sisi
akinamama na vijana ndio tulio wengi na tegemeo la Chama chetu kukipatia
ushindi wa kishindo, nasaha zangu nyote utakapofika wakati mtekeleze wajibu
wenu”, alisema.
Aidha, Mama Mwanamwema
aliwataka washiriki na wananchi wote kushrikiana an Serikali katika kuwafichua
watu wote wanaojihusisha na vitendo vya udhalilishaji dhidi ya wanawake na
watoto.
Alisema udhalilishaji wa
kijinsia pamoja na matumizi ya dawa za kulevya
ni mambo yanayohitaji mikakati mizuri ya haraka katika kupambana navyo.
Alisema kuna umuhimu wa
kuangalia na kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ambapo chanzo chake
kinatokana na mmong’onyoko wa maadili katika jamii.
“Naamini mada ya mmong’onyoko
wa maadili itakapowasilishwa mtapata kuzungumza kwa kina, na kwa mifano na
hatimae kupendekeza mbinu za kuihami jamii yetu”, alisema.
Aidha, alitowa wito kwa
viongozi wa dini, wanasiasa, vyombo vya habari, viongozi wa taasisi za kiraia
na Jumuiya zisizo za Kiserikali kuzidi kuwaelimisha wananchi ju ya athari na
ubaya wa vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto.
Alieleza matumaini yake
kuwa kutokana na mafunzo hayo, vita dhidi ya vitendo vya udhalilishaji na
ukiukwaji wa maadili, vitapata kasi mpya, hivyo akaiomba jamii kushirikiana na
Serikali.
Katika hatua nyengine, Mama
Mwanamwema aliipongeza UWT kwa maandalizi ya Kongamano hilo, ikiwa ni
utekelezaji wa majukumu yake ya msingi.
Aliwapongeza
wajasiriamali walioshiriki katika kongamano hilo, kwa kuunga mkono juhudi za
Serikali katika kufanikisha azma yake ya kuinua kipato na hali za wananchi wake.
Aidha, alitoa pongezi za
dhati kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed
Shein kwa hatua mbali mbali anazozichukuwa katika kuhimiza na kuwasidia
wajasiriamali, ikiwa pamoja na kuanzisha mfuko wa Uwezeshaji wananchi kiuchumi
ambao hutoa mikopo nafuu kwao.
“Ni vyema mkautumia mfuko
huo kikamilifu katika kujiongezea mitaji kwenye biashara zenu na kukuza
maendeleo kwa ujumla”, alisema.
Mama Mwanamwema aliwataka
washirki wa kongamano hilo kuwa makini na watulivu katika kipindi chote cha
mafunzo ili kufikia malengo yaliokusudiwa, sambamba an kuwapongeza wafadhali
mbali mbali waliowezesha kufanyika kongamano hilo.
Nae, Waziri wa Kazi,
Uwezeshaji, Wazee, wanawake na watoto Moudline Castico, alimpongeza Mama
Mwanamwema kwa mchango mkubwa anautowa katika kusaidia harakati za ujasiriamali
kwa akinamama.
Aidha, Makamo Mwenyekiti
wa UWT Taifa, Thuwayba Edington Kisasi, alisema ni lengo la Jumuiya hiyo kuhakikisha
wananchi wote wanapata elimu ya ujasiriamali nchi nzima.
Aliwataka washirkki wa
mkongamano hilo kuitafutia ufumbuzi changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia,
akibainisha chanzo chake kinatokana na jamii kuondokana na utamaduni, mila na
silka za Wazanzibari.
Alitumia furs ahiyo kuwapongeza
wafadhali mbali mbali, ikiwemo ZRB, NMB, ZSSF, ZURA, Bima, Chuo Kiku cha Taifa
SUZA na wengineo kwa michango yao iliyofanikisha kufanyika kongamano hilo.
Mapema, katika hafla hiyo
Mama Mwanamwema aliangalia bidhaa mbali mbali zinazozalishwa na vikundi vya
ujasiriamali kutoka Mikoa hiyo ya Unguja.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment