Habari za Punde

Vitambilisho vipya vya Mzanzibari kuzinduliwa kesho

 Mkurugenzi Mtendaji ,Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar Dkt.Hussein K. Shaaban akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali kuhusu uzinduzi wa vitambulisho vipya ambavyo vitakuwa na "Chip" (Smart Cards) huko katika Ukumbi wa Wizara  ya Habari Utalii na Mambo ya kale Kikwajuni.

Baadhi ya Waandishi pamoja na Maofisa wa Wakala wa Usajili na Matukio  wakimsikiliza  Mkurugenzi Mtendaji ,Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar  Dkt.Hussein K.Shaaban (ambae hayupo pichani ) kuhusu uzinduzi wa vitambulisho vipya ambavyo vitakuwa na "Chip" (Smart Cards) huko katika Ukumbi wa Wizara  ya Habari Utalii na Mambo ya kale Kikwajuni..
Picha na Khadija Khamis -Maelezo Zanzibar,

Na Miza Kona Maelezo Zanzibar      
Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar kesho wanatarajiwa vitambulisho vipya vya Mzanzibar huko katika ukumbi wa Shekh Idrisa Abdulwakili Kikwajuni Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari huko katika ukumbi wa Wizara ya Habari na Mambo ya Kale Mkurugenzi Mtendaji Dr. Hussein Khamis Shaaban amesema vitambulisho  vitaanza kutolewa kwa awamu tofauti kwa wananchi wote.
Uzinduzi huo wa utoaji wa vitambulisho vipya unatokana na kukamilika kwa zoezi zima la mfumo mpya wa usajili wa uimarishaji wa taarifa za vitambulisho ili kuwa na hadhi na ubora.
Amefahamisha kuwa vitambulisho hivyo  ni vyenye  ubora ambavyo vitatumika kwa matumizi mengi kutokana na uwezo wake wa kubeba  program mbalimbali za smat card.
Akizitaja program hizo ni pamoja na kuwa  taarifa mama za utambulisho na alama za kibayolojia, taarifa za leseni ya udereva, taarifa muhimu za huduma za kiafya pamoja na  kutumika katika miamala ya kifedha.
Mkurugenzi huyo alifafanua  kwamba vitambusho hivyo vitatumika katika program hizo  pale mtumiaji atakapopoteza moja ya kitambulisho chake  anachotumia kwa kufuata sheria zilizowekwa.
Aidha amewasisitiza wananchi kuvienzi na kuvitunza vitambulisho hivyo kutokana na ubora wake ili kuepuka usumbufu na gharama zaidi kwa kuleta maendeleo nchini.
Uzinduzi huo utafanyika kesho  saa 3.00 asubuhi  Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.