Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza
na Maafisa Michezo wa Mikoa na Halmashauri za Tanzania Bara wakati akifungua kikao
kazi cha maafisa hao cha siku mbili (tarehe 12-13, Desemba 2019) leo Jijini
Dodoma. Kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Michezo kwa Afya, Ajira na Maendeleo
ya Viwanda”
Na. Anitha Jonas –
WHUSM, Dodoma.
Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka Maafisa Michezo
kote nchini kulinda viwanja vya michezo
na kutoa taarifa ya viwanja vya michezo vinavyobadilishwa matumizi hata kwa
siri.
Waziri Mwakyembe
ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma wakati akifungua Kikao Kazi cha Maafisa
Michezo kinachofanyiki kwa siku mbili chenye lengo la kutathimini, kujadili na
kuelekezana namna bora ya kuimarisha michezo na kutumia sekta hiyo kutangaza
vivutio vya utalii nchini.
"Wapo baadhi ya
Wakuu wa shule na walimu wanaozuia michezo shuleni na mnawajua, mnakaa kimya
sasa wajibu wenu ni nini? Tambueni michezo sasa ni ajira ambayo ni mgodi na
taifa lina vijana wengi simamieni vyema michezo,'' Dkt. Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza
katika ufunguzi wa kikao kazi hicho Dkt. Mwakyembe amekiagiza Chuo cha Michezo cha
Malya kufanya utafiti wa kodi inayotokana na michezo mbalimbali inayofanyika
nchini.
Naye Kaimu Katibu
Mkuu Dkt. Ally Possi amemwagiza Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Yusuph
Singo kukakikisha kikao kazi hicho kinakuwa endelevu na kufanyika kila mwaka. Aidha,
aandae utaratibu wa kuwa na vikao hivyo kikanda vikiwa na lengo la kuwaandaa
vijana waweze kushiriki michezo mbalimbali kitaifa na kimataifa.
"Kikao Kazi hiki
kitatoa tathimini ya wapi tulipo, nini kifanyike pamoja na kutoa mwongozo wa
kusimamia michezo mbalimbali na kutoa maelekezo kwa kuweka maazimio
yatakayosaidia kupeleka michezo kuwanufaisha vijana maana michezo ni
ajira," alisema Dkt. Possi.
Aidha, Dkt. Possi
aliwataka maafisa michezo hao kuzingatia mada ya uandishi wa maandiko ya
udhamini katika michezo ambayo ni kichocheo cha kufanikisha michezo nchini
kwani maandiko mradi hufanyika ni miongoni mwa kazi inayofanyika kila siku katika
sekta ya michezo, hivyo ni vyema kuwa na
ujuzi huo.
Naye Mkurugenzi wa
Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini Yusuph Singo alitoa pongezi na shukrani kwa
Makatibu Tawala Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa na Halmashauri
kwa kuwawezesha maafisa michezo hao kushiriki kikao hicho kwa mikoa yote nchini
imeshiriki.
Akitoa neno la
shukrani kwa niaba ya washiriki wa kikao kazi hicho Afisa Michezo kutoka Wilaya
ya Mbarali Bw. Gerald Chiwaya aliishukuru wizara kwa kuandaa kikao hicho ambacho
kimefanyika kwa mara ya kwanza nchini ambacho kina washiriki 265 kutoka mikoa
yote Tanzania Bara.
Kaimu
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Ally Possi akitoa
maelezo mafupi kuhusu Kikao kazi cha Maafisa Michezo wa Mikoa na Halmashauri za
Tanzania Bara kinachofanyika kwa siku mbili (tarehe 12-13,Desemba 2019) leo
Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Michezo kwa Afya, Ajira na
Maendeleo ya Viwanda”
Mkurugenzi
Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw.Yusuph Singo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo akitambulisha washiriki wa Kikao kazi cha Maafisa Michezo wa Mikoa
na Halmashauri za Tanzania Bara wakati wa ufunguzi wa kikao kazi hicho cha siku
mbili (tarehe 12-13,Desemba 2019) leo Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya kikao kazi
hicho ni “Michezo kwa Afya, Ajira na Maendeleo ya Viwanda”
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja
na Viongozi wa Wizara mara baada ya kufungua Kikao Kazi cha Maafisa
Michezo wa Mikoa na Halmashauri za
Tanzania Bara cha siku mbili (tarehe 12-13,Desemba 2019) leo Jijini Dodoma.
Kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Michezo kwa Afya, Ajira na Maendeleo ya
Viwanda”
Waziri
wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati
waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Michezo mara baada ya kufungua Kikao Kazi cha Maafisa
Michezo wa Mikoa na Halmashauri za Tanzania Bara cha siku mbili (tarehe 12-13 Desemba
2019) leo Jijini Dodoma. Kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Michezo kwa Afya,
Ajira na Maendeleo ya Viwanda”
(Picha
na Shamimu Nyaki, WHUSM, Dodoma)
No comments:
Post a Comment