WAKILI
Suzana Senso akizungumza wakati akitoa mada ya nafasi ya mwanamke kwenye urithi wa mirathi maadhimisho ya siku ya wanawake duniani iliyofanyika kwenye viwanja vya Nkende Manispaa ya Musoma mjini
iliyokuwa na kauli mbiu ya Kizazi cha Usawa kwa maendeleo ya Tanzania ya
Sasa nay a Baadae
MEZA Kuu wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye maadhimisho hayo kushoto ni Mwenyekiti wa UWT
Taifa Gaudance Kabaka akifuatiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara
Caroline Matapula na Mkurugenzi wa Musoma Mjini Mjovela na kulia ni Wakili Suzana Senso
MEZA Kuu wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye maadhimisho hayo
WAKILI
Suzana Senso wa pili kutoka kulia akishiriki kucheza na wakina mama wengine wakati wa maadhimisho hayo.
NA MWANDISHI WETU,MUSOMA.
WAKILI
Suzana Senso amesema kwamba hata wanawake wanaweza kuandika mirathi ili
kupunguza msongamano wa kesi za kugombania mali kwenye jamii pindi
wanapokuwa wakitangulia mbele za haki.
Senso aliyasema hayo
wakati akitoa mada ya nafasi ya mwanamke kwenye urithi wa mirathi huku
akisisitiza wanawake kujituma na kutafuta mali kutokana na kuwepo kwa
dhana potofu kwamba wanapotafuta hakuna watakaonufaika na mali hizo
pindi wanapofariki .
Maadhimisho ya siku ya wanawake dunia
iliyofanyika kwenye viwanja vya Nkende Manispaa ya Musoma mjini
iliyokuwa na kauli mbiu ya Kizazi cha Usawa kwa maendeleo ya Tanzania ya
Sasa nay a Baadae.
Mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa UWT
Taifa Gaudance Kabaka ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara
Caroline Matapula,Madiwani wa Viti Maalumu wa Manispaa ya Musoma,Afisa
Maendeleo ya Jamii mkoa huo na Mwakilishi wa Mbunge Anna Makilanga na
Mwakilishi kutoka Takukuru.
Wakili Senso alisema kwamba sheria
ya mirathi inasema kama mke akifariki na kumuacha mume na watoto mume
hupata moja ya tatu ya mali za marehemu mkewe na mbili ya tatu huenda
kwa watoto.
Alisema kwamba pia ikitokea mke amefariki na
amemuacha mume lakini hakuna watoto inaangaliwa kama kuna ndugu ikiwa
wapo ndugu hao wa mke hutakiwa kupata nusu ya mali na nusu inayobakia
huenda kwa mume kwa hiyo ndugu wa mwanamke ambao ni marehemu hupata sawa
kwa sasa na mume wake aliyeachwa.
“Lakini
ikiwa mwanamke ndiye amefariki na hakuacha ndugu yoyote wala mtoto
yeyote isipokuwa kumuacha mume haturudhi mali zote za Mkwe”Alisema
Akizungumza
katika maadhimisho yalikwenda sambamba na wakina mama wajasiriamali
kuonyesha bidhaa zao ambapo mgeni rasmi Mama Kabaka alionyesha
kufarijika alipokuta wakina mama wanapiga vita umaskini kwa
kujishughulisha na biashara.
Pia maadhimisho hayo yalihudhuriwa
na Benki tofauti tofauti ikiwemo NMB, NBC na Kampuni za simu ikiwemo
TTCL pia kwenye maonyesho hayo kulikuwa na dawati la jinsia ambalo
lilitoa elimu kwa wananchi walikuwa wamehudhuria.
No comments:
Post a Comment