Mkuu
wa Idara ya Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa
Magonjwa ya Wanawake, Enid Chiwanga (kushoto) akiongea na ujumbe wa THBUB
(mbele yake) uliotembelea Hospitali ya rufaa
jijini Dodoma
Kamishna
wa THBUB, Dkt. Fatma Khalfan (kulia) na Kamishna Amina Talib Ali (kushoto)
wakitoa mkono wa pole kwa mmoja wa wazazi waliojifungua katika Hospitali ya
rufaa jijini Dodoma walipotembelea
kuwaona wagonjwa
Ujumbe
wa THBUB ukiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Wanawake
na Uzazi, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake, Enid Chiwanga
(katikati) huku wakionyesha ishara ya “mwanamke hodari”muda mfupi mara baada ya
ujumbe wa THBUB kumaliza ziara yake katika hospitali hiyo.
Na
Mbaraka Kambona,
Katika
kuelekea kilele cha kuadhimisha siku ya wanawake duniani, ujumbe wa wanawake
kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) umetembelea Idara ya
Magonjwa ya Wanawake na Uzazi iliyopo katika
Hospitali ya rufaa jijini Dodoma
mapema leo Machi 6, 2020.
Ujumbe
huo uliotembelea hospitali hiyo uliongozwa na Makamishna
wawili, Dkt. Fatma Khalfan na Amina Talib Ali kwa lengo la kuwafariji wakina
mama wagonjwa na wazazi waliolazwa katika hospitali hiyo.
Kamishna
wa THBUB, Dkt. Fatma Khalfan akiongea wakati wa kukabidhi bidhaa mbalimbali
walizopeleka kwa ajili ya wagonjwa alisema kuwa lengo la ziara yao ni kwenda
kuwafariji wagonjwa kina mama katika hospitali hiyo kwa kuzingatia wiki hii ni ya kuadhimisha siku ya mwanamke
duniani.
Dkt.
Fatma alisema kuwa Afya ni muhimu sana kwa mwanadamu na kwamba jamii haitaweza
kujenga uchumi wake kama watu wake hawana afya nzuri.
Aliongeza
kwa kusema kuwa kwa niaba ya uongozi wa THBUB wanaipongeza serikali kwa
jitihada zake za makusudi katika kuboresha sekta ya afya nchini hususani
matibabu mazuri kwa kina mama na watoto.
Alisema
kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli imeendelea
kutekeleza utoaji wa haki ya afya kwa vitendo kwa kuendelea kuboresha na kujenga
miundo mbinu mbalimbali ya zahanati na vituo vya afya ikiwemo kuongeza bajeti
ya ununuzi wa dawa nchini.
Aidha, Dkt. Fatma alisema kuwa pamoja na
jitihada kubwa za serikali katika kuboresha sekta ya afya bado kuna changamoto
ambazo zinaikabili sekta hiyo na hivyo kutoa wito kwa wadau kushirikiana pamoja
na serikali katika kutatua changamoto
hizo.
Mkuu
wa Idara ya Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa
Magonjwa ya Wanawake, Enid Chiwanga wakati akiupokea ujumbe huo alitoa shukrani
kwa uongozi wa THBUB kwa uamuzi wao wa kutembelea wagonjwa katika hospitali
hiyo na kusema kuwa wamefarijika kwani ziara hiyo itatoa tumaini jipya kwa
wagonjwa waliopo katika hospitali hiyo.
Kilele
cha maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani mwaka huu ni Machi 8, 2020 na kwa
mwaka huu maadhimisho hayo yanaenda sambamba na kumbukizi ya miaka 25 tangu
wanawake wakutane katika mkutano wa Beijing nchini China mwaka 1995.
No comments:
Post a Comment