Habari za Punde

Zoezi la Uhakiki Vyama vya Siasa Laanza kwa Mafanikio

Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa, Bw. Sisty Nyahoza akifafanua jambo mbele ya viongozi wa Kitaifa wa Chama cha United Democratic Party (UDP) wakati wa zoezi la uhakiki wa vyama vya siasa walipotembela Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa UDP Taifa, John Momose Cheyo.
Mhazini wa Chama cha Wakulima (AAFP), Bw. Ndonge Said Ndonge akitoa maelezo kuhusu namna wanavyo tunza taarifa zao za mapato namatumizi mbele ya Maafisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) walipofika katika Ofisi za Makao Makuu ya chama hicho kwa ajili ya zoezi la uhakiki lililoanza leo jijini Dar es Salaam.
Maafisa Kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) wakipitia nyaraka ya fedha za Chama cha Wakulima (AAFP) wakati wa zoezi la uhakiki wa vyama vya siasa lililoanza leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Gharama za Uchaguzi na Ruzuku, Bi. Hollo Kazi, Afisa Mipango wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP), Bw. Emmanuel na Mkaguzi wa Ndani Bw. Mussa Boma.
Mkuu wa Idara ya Gharama za Uchaguzi na Ruzuku toka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bi. Hollo Kazi akielezea jambo mbele ya viongozi wa Kitaifa wa Chama cha Wakulima Tanzania (AAFP) wakati wa zoezi la uhakiki wa vyama vya siasa walipotembela Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Mipango wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP), Bw. Emmanuel Msengi.
(Na: Mpiga picha wetu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.