Habari za Punde

ZEC ina wajibu wa kuwa karibu na wananchi


Na Jaala Makame Haji, ZEC

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC imesema  itaendelea na utaratibu wa kuimarisha majengo ya ofisi za uchaguzi za wilaya pamoja na kujenga majengo mapya ambayo yatasaidia wananchi kupata huduma za kiuchaguzi katika maeneo ya karibu na makazi yao.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe.Jaji Mkuu Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid ameyasema hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la ofisi ya uchaguzi ya wilaya ya Magharibi “A” iliyopo Mwera Mkoa Mjini Magharibi.

Amesema, Tume ya Uchaguzi inawajibu wa kuwa karibu na wananchi wake ili kufikia dhamira ya ushiriki wa wananchi katika hatua zote za uchaguzi nchini.

 Mkurugenzi wa Uchaguzi Thabit Idarous Faina amesema kuwepo kwa jengo hilo kutarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi wa Magharibi “A” hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020.

Afisa  Uchaguzi  wa wilaya hiyo Suluhu Ali Rashid amewata wananchi kuwa na utaratibu wa kuzitumia ofisi za uchaguzi za wilaya hatua ambayo itasaidia upatikanaji wa taarifa sahihi.

Ujenzi wa jengo la ofisi ya uchaguzi ya wilaya ya Magharib “A” unasimamiwa na fundi dhamana mzalendo Mohamed Mkuta kutoka Kampuni Ya Trip Construction limited iliyopo Kijito Upele Zanzibar

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.