Habari za Punde

Waziri Mkuu ashiriki katika tukio la kuvunjwa kwa Baraza la Wawakilishi Zanzibar

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Baraza la Wawakilishi, Zubeir Ali Maulid (kulia) na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Raya Issa Musellem  wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Baraza la Wakilishi  kushiriki katika tukio la kuvunjwa kwa Baraza hilo kulikofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt, Ali Mohammed Shein, Juni 20, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Rais wa Zanzibar n a Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  baada ya kuvunja Baraza la Wawakilishi kwenye ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Juni 20, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi (wa pili kushoto wakizungumza na Spika wa baraza la Wawakilishi,  Mhe. Zubeir Ali Maulid  (kulia) baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein kuvunja Baraza la Wawakilishi kwenye ukumbi wa Baraza hilo Juni 20, 2020.  Wa pili kulia ni Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Raya Issa Msellem. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.