BAKAR
MUSSA –PEMBA.
WANANCHI
wa mikoa miwili ya Pemba, wamejitokeza katika vituo mbali mbali
walivyojiandikisha kuchukuwa vitambulisho vya kupigia kura ili kujiweka tayari
kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo baadae.
Akizungumza
na Waandishi wa habari huko katika kituo cha uchukuaji wa vitambulisho hivyo katika Skuli ya Chanjamjawiri , Makamo mwenyekiti wa
Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Zanzibar, Mabrouk Jabu Makame, alisema zoezi liko vizuri watu
wamejitokeza kwa utulivu mkubwa huku kukiwa na utaratibu mzuri ambao kila mmoja
anaweza kupata kitambulisho bila ya usumbufu.
Alieleza
kuwa Vitambulisho hivyo vimeanza kutolewa na Tume hiyo kupitia vituo mbali
mbali ili kupunguza msongomano watu kwani kwa yule ambae hatopata ndani ya
Vituo vyao atapatiwa katika vituo vya Tume ya Uchaguzi zilizoko kila Wilaya .
Makamo
mwenyekiti huyo, aliwataka watendaji kuwa na uharaka pale mwananchi anapoingia
katika chumba cha kuchukulia kitambulisho ili waepukane kutopoteza muda mwingi
.
“
Tume inawashukuru Wananchi wa Pemba, kwa kujitokeza kwa wingi katika vituo
hivyo kwa ajili ya kuchakuwa vitambulisho vyao na kuweka utaratibu mzuri wa
foleni zinazowafanya wapate haki yao hiyo kwa urahisi zaidi,”alisema.
Mussa
Kombo Mussa mkaazi wa Matale Chake Chake Pemba, alisema wameweka utaratibu
mzuri wa kupeena namba kwa kila anaefika ili kuwafanya wananchi wasipate tabu
na hilo limewafanya wapate vitambulisho vyao kwa muda mfupi tokea kuingia
kituoni.
Aliwataka
Wananchi wenzake kujitokeza kwa wingi kuchukuwa vitambulisho vyao na wavione
kuwa hiyo ni mali yao ambayo itawafanya waweze kupiga kura kwa kumchagua
kiongozi wanaemtaka kwa maslahi ya nchi yao.
“
Huwezi kupiga kura kama huna Kitambulisho cha kupigia kura , nawasihi Wananchi
wenzangu tujitokeze kuvichukuwa ili tusije tukalalamika baadae,”alisema.
Nae
bibi Ramla Abas Siwatu , mkaazi wa Matale alisema utaratibu unaotumika katika
kuchukuwa vitambulisho ni mzuri kwani ni muda mdogo tu wakuingia chumbani na
kupatiwa kitambulisho chako.
“
Mimi na wenzangu tumekuja mapema tokea saa
12 za asubuhi , ingawaje tulikuwa tunajuwa vituo vitafunguliwa saa 2 ,
hii ili tupa imani kuwa tupate mapema lakini tunashukuru baada ya kufunguliwa
tu , tulipata bila ya usumbufu,”alieleza.
Hanifa
Juma Khamis wa kituo cha Skuli ya
Chanjamjawiri , alieleza kuwa wanashukuru kuwa vitambulisho wanapatiwa bila ya
usumbufu ingawaje watu ni wengi waliojitokeza katika siku hiyo ya kwanza
kufuata haki yao hiyo .
Aliwataka
wananchi wenzake kuacha dharau wajitokeze kuchukuwa vitambulisho hivyo kwani
ndio silaha pekee ya kuwapeleka katika kuchaguwa Viongozi wanaowapenda.
Zainabu
Moh’d Karenga, kituo cha Wawi Chake Chake Pemba, amesema wanashukuru utaratibu
unaotumika kwa kuchukuwa vitambulisho vya mpiga kura ni mzuri kiasi ambacho
wanapoingia vituoni tu wanapatiwa haki hiyo bila ya usumbufu wowote.
Nae
Nassor Iddi Suleyum wa kituo cha Vikunguni,alieleza kufurahishwa kwake na
utaratibu unaotumiwa na Tume ya Uchaguzi ya ZEC juu ya kuwapatia vitambulisho
vya mpiga kura na kuwataka wananchi ambao hawajajitokeza kufanya hivyo ili
kujiweka tayari na Uchaguzi.
Zoezi
la ugawaji wa vitambulisho vya kupigia kura limeanza tarehe 18 na linatarajiwa kumalizika tarehe 19/7 mwaka huu kwa Pemba na wale ambao watakosa kuvipata
vituoni humo wanatakiwa kuvifuata katika Ofisi za Uchaguzi Tume ya Uchaguzi za kila Wilaya.
No comments:
Post a Comment