Habari za Punde

Zantel Yazindua Duka Jipya Lililopo Vuga, Wazingatia Afya za Wateja Wao.

Wateja wa Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel wakipata huduma katika Duka jipya la Zantel la Vuga baada ya kuboresha  na kufanyiwa matengenezo makubwa ili kutowa huduma bora kwa wateja wao. na kuzingatia ushauri wa Wataalam wa Afya. 
Mfanyakazi wa Duka la Zantel Vuga Jijini Zanzibar akitowa huduma kwa mtaji wa kampuni hiyo alipofika kupata huduma hiyo.  


ZanzibarJulai 1, 2020. Wateja wa Zantel waliopo Zanzibar sasa watafurahia kupata huduma za mawasiliano zilizoboreshwa zaidi katika duka jipya la Zantel lililopoVuga Jijini baada ya kufanyika kwa maboresho ili kukidhi mahitaji ya wateja.

Duka hilo la kisasa limezingatia pia afya za wateja kwa kuwekewa miundombinu mbalimbali kwa ajili ya kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona (Covid-19) ikiwamo sehemu maalumu za kuoshea mikono pamoja na ukaaji foleni wa kuzingatia umbali wa mita mbili.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Zantel - Zanzibar.Ndg. Mohamed Khamis Mussa Baucha alisema duka hilo lenye zaidi ya miaka 20 limeboreshwa kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia ili kukidhi mahitaji ya huduma kwa wateja wake.

“Hili duka tumelifanyia ukarabati wa hali ya juu ili liwe imara na tumeliimarisha katika nyanja zote. Sisi mara zote tunasikiliza kero za wateja wetu na moja ya kero ilikuwa ni foleni hivyo tumeleta mfumo maalumu wa kukaa kwenye foleni (Queuing system) ambao utapunguza msongamano,” alisema.

Mfumo huo unaruhusu mteja kujisajili kwenye mtambo maalum na kupewa namba atakayoitumia wakati anasubiri huduma kwenye foleni na ataitwa mara tu zamu yake itakapofika hali inayofanya kuwa na ufanisi wa huduma.

Vile vile, duka hilo linauwezo wa kutoa huduma kwa wateja zaidi ya 100 kwa siku na kwamba kwa maboresho hayo wataweza kuhudumia wateja wengi zaidi kwa haraka zaidi.

“Nategemea tutahudumia wateja wengi zaidi kwa haraka kwa hiyo nawakaribisha wateja waje wajionee duka jipya na la kisasa ambalo ni duka la kwanza la Zantel Unguja,” alisema Meneja wa Maduka ya  Zantel Zanzibar.Bi. Mwajuma Senkanga.

Huduma zinazopatikana dukani hapo ni pamoja na huduma ya Ezypesa, kusajili namba za simu, pamoja na bidhaa za mawasiliano kama vile simu.

 Kuhusu Zantel

Zantel ni Kampuni inyaoongoza kwa utoaji wa huduma za mawasiliano Visiwani Zanzibar kwa miaka mingi hivi sasa ikiongoza kwa ubora wa miundombinu ya mawasiliano, huduma pamoja na bidhaa.

Huduma ya kifedha ya Ezypesa ni ya kwanza nchini Tanzania kutoa huduma za kibenki za kawaida pamoja na za kiislamu kwa ushirikiano na benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ).

Aidha, Zantel ni kampuni inayoongoza kwa utoaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania kupitia uwekezaji kwenye teknolojia ya fibre optic cable ambayo inaiunganisha Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki na duniani umeiwezesha Kampuni hiyo kuleta mapinduzi ya haraka ya kidigitali hapa nchini.

Aidha, Miundombinu hiyo imeiwezesha Zantel kutoa huduma za kimataifa za sauti na data kwa jumla kwa kampuni nyingine na nchi jirani hivyo kuchagia ukuaji wa teknolojia ya digitali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.