Habari za Punde

Mwenyekiti Mstaaf wa CCM Mkoa wa Mjini Ndg. Borafia Silima Awanadi Wagombea wa Jimbo la Magomeni KwaTiketi ya CCM na Kuwaombea Kura.

Mwenyekiti mstaafu wa Mkoa wa Mjini Kichama Borafya Silima akizungumza na Wanachama wa chama cha Mapinduzi Jimbo la Magomeni kuhusu Kuwachagua viongozi watakaoleta maendeleo katika Mkutano wa kampeni wa kuwanadi Wagombea wa Jimbo hilo huko Uwanja wa Jitini Magomeni 
Baadhi ya Wagombea wa Jimbo la Magomeni wa Chama cha Mapinduzi wakifatilia kwa makini Mkutano wa kampeni wa kuwanadi Wagombea wa Jimbo hilo huko Uwanja wa Jitini ulioko Magomeni.

Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakishangilia katika Mkutano wa kampeni wa kuwanadi Wagombea wa Jimbo la Magomeni huko Uwanja waJitini ulioko Magomeni.

Picha na Maryam Kidiko- Maelezo Zanzibar

Na.Mwashungi Tahir   Maelezo Zanzibar.

MWENYEKITI  Mstaafu wa Mkoa wa Mjini Kichama Borafya Silima  amewataka wanachama wa jimbo la Magomeni kuwachagua viongozi wanaofaa ili waweze kuleta maendeleo  katika jimbo hilo.


Ameyasema hayo huko katika uwanja wa Jitini ulioko  Jimbo la Magomeni wakati alipokuwa kwenye mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi akiwanadi wagombea wa Ubunge. Wawakilishi na Madiwani.


Amesema Chama cha Mapinduzi  ni chama ambacho  kina utaratibu  wa mipango  pamoja na maazimio mahsusi ya kufanya kazi zake za kuwaletea wananchi wake  maendeleo kwa kutekeleza ilani .


“Chama cha Mapinduzi ni chama ambacho kinafuata utaratibu wa kuleta  maendeleo kwa wananchi kwa kutekeleza ilani”, alisema mwenyekiti huyo.


Aidha alisema wanachama wa chama hicho  wanampongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein katika awamu ya saba  kwa kutekeleza vyema majukumu yake na kutimiza ahadi zake kwa kipindi cha miaka kumi.


Hivyo amewataka  wananchi wa jimbo hilo kuwapa ridhaa wagombea hao ili waweze kuleta mabadiliko ikiwemo kuimarisha njia za ndani , kuhakikisha  maji safi na salama yanapatikana pamoja na    kuwawezesha akinamama katika vikundi vya ujasiriamali na mambo mengine mengi ya maendeleo.


Pia amewaomba wanachama wa jimbo la Magomeni  kutoa mashirikiano kwa viongozi kwani chama cha Mapinduzi kinapenda umoja na mshikamano ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.


Nae Mwenyekiti wa  CCM Jimbo hilo Mahmoud Juma Ali amewaasa vijana kuepuka kushawishiwa na watu wasiotaka maendeleo na kuwa makini ili ifikapo tarehe 28 mwezi huu kushiriki kwenda kupiga kura kwa kuchagua chama cha Mapinduzi ili kiweze kuleta ushindi kwa kishindo.


Nao viongozi hao wakinadi sera zao wameahidi iwapo watapewa ridhaa na kuingia madarakani watahakikisha changamoto zinazowakabili  wananchi katika jimbo hilo kwa kuhakikisha  watasimama imara na kuwa  mstari wa mbele katika kuzitatua ili jimbo hilo liweze kuimarika zaidi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.