Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi akutana na Baba Askofu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Jijini Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Baba Askofu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Jijini Zanzibar Askofu  Michael Hafidh, alipofika Ikulu kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi huo leo 26-1-2021.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Baba Askofu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Jijini Zanzibar Askofu Michael Hafidh (kulia kwa Rais) akiwa na ujumbe wake Ndg.Edwin Mkwaya na Ndg.Luis Majaliwa, walipofika Ikulu kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi  akiagana na Baba Askofu wa Kanisa la Anglikana Jijini Zanzibar Askofu Michael Hafidh baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibaer na (kushoto kwa Rais) Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said.
 

Rais Dk. Mwinyi alikutana na Baba Askofu Michael Henry Hafidh ambapo katika maelezo yake alimpongeza Askofu huyo pamoja na Waumini wote wa Kanisa la Anglikana kwa kuendelea kuiombea nchi amani.

Pamoja na hayo, Rais Dk. Mwinyi alizipongeza juhudi za uongozi wa Kanisa hilo la kutaka kujenga Chuo cha Amali huko kisiwani Pemba pamoja na azma yao ya kutaka kuekeza katika eneo la Kiungani  Jijini Zanzibar.

Mapema Baba Askofu alimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa ushindi mkubwa alioupata na kueleza matumaini makubwa waliyonayo wananchi wa Zanzibar kutokana na uongozi wake huku akimpongeza kwa kuwepo kwa maridhiano na hatimae kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.