Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi Asaini Kitabu cha Maombolezi na Kutoa Mkono wa Pole kwa Mama Janeth Magufuli leo.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisaini kitabu cha maombolezi ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt.John Pombe Magufuli,hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam leo 19-3-2021

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiondoka katika viwanja vya Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam baada ya kusaini kitabu cha maombolezi cha Hayati Dkt. John Pombe Magulili aliyekuwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakimfariji Mjane wa hayati aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli Mama Janeth Magufuli alipofika Ikulu Jijini Dar es Salaam kutowa mkono wa pole kwa familia ya marehemu
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakimfariji Mjane wa hayati aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli Mama Janeth Magufuli alipofika Ikulu Jijini Dar es Salaam kutowa mkono wa pole kwa familia ya marehemu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametia saini kitabu cha maombolezi ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dk. John Joseph Pombe Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021.

Rais Dk. Mwinyi ametia saini kitabu hicho cha maombolezi huko katika viwanja vya ukumbi wa Karimjee, ulioko Jijini Dar es Salaam na kueleza jinsi alivyopokea kwa mshtuko mkubwa kifo cha kiongozi huyo.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi alieleza jinsi Hayati Rais Magufuli alivyoitumia nchi kwa nidhamu kubwa sana ikiwa ni pamoja na kusimamia  kiuchumi na kimaendeleo kwa misingi ya amani, utulivu, umojana mshikamao.

Mapema  Rais Dk. Mwinyi alimfariji na kumpa pole Mjane wa Hayati Rais Dk. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huko Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Dk. Mwinyi akiwa na Mama Mariam Mwinyi walimpa pole Mjane wa Marehemu Hayati Magufuli Mama Janet Magufuli na kumtaka awe na subira yeye pamoja na familia yake katika kipindi hichi kigumu cha msiba.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.