Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiwasili katika viwanja vya Ikulu Chamwino Dodoma kuhudhuria hafla ya kuapishwa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mteule Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango.hafla hiyo imefanyika leo jioni 31-3-2021. wakiongozana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt.Bashiri Ally.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama wakati ukipigwa wimbo wa Taifa wakati wa hafla ya kuapishwa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mteule Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango katika viwanja vya Ikulu Chamwino Jijini Dodoma leo.
Mhe. Philip Isdor Mpango akilia kiapo cha kuwa
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla hiyo imefanyika
katika viwanja vya Ikulu Chamwino Jijini Dodoma leo 31-3-2021
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof.Ibrahim Hamis Juma
akimuapisha Mhe. Philip Isdor Mpango
kuwa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla hiyo ya
kuapishwa imefanyika katika viwanja vya Ikulu Chamwino Dodoma leo 31-3-2021
No comments:
Post a Comment